Skip to main content

UHARIBIFU WA MAZINGIRA WAPELEKEA WAKAZI WA MPWAPWA DODOMA KUKOSA MAJI

Image result for UHARIBIFU WA MISITU MPWAPWA DODOMA
         

Kufuatia uharibifu mkubwa wa mazingira katika wilaya ya Mpwapwa mkoani Dodoma ambao umekuwa ukifanywa na  wakazi wa wilaya hiyo imepelekea wakazi wa baadhi ya vijiji wilayani humo kukosa huduma ya maji.

Hayo yameelezwa leo  wilayani humo  na Mwenyekiti wa Kijiji cha Idilo kilichopo  Kata ya  Mazae  bw, ROBERT  NJAMASI  wakati akizungumza na DODOMA FM kupitia Taswira ya habari.

 NJAMASI amesema kuwa hivi sasa  wakazi wa vijiji vya Idilo,Mazae na Chamhawi wamekuwa wakifanya uharibifu wa mazingira kwa kufyeka miti ikiwa ni pamoja na kulima katika vyanzo vya maji.

Aidha kutokana na kuwepo kwa hali hiyo ameiomba Serikali kuongeza faini pamoja na kifungo cha muda mrefu kwa wananchi watakaobainika kuharibu mazingira ili  kukomesha vitendo hivyo.

Kwa upande  wake Afisa Mazingira wa Wilaya ya Mpwapwa,THEODORY MULOKOZI amebainisha kuwa, wameamua kuchukua hatua ili kumaliza tatizo hilo kwa kuunda kikosi kazi  cha wilaya ambacho kitakuwa na wataalam mbalimbali wa Mazingira akiwemo Mkuu wa wilaya hiyo.

Hata hivyo Afisa huyo ameiomba Serikali kutilia mkazo suala la utunzaji wa mazingira hususani katika wilaya hiyo ambayo imekuwa na vyanzo vingi vya maji lakini vimekuwa haviwanufaishi wakazi wa Wilaya ya Mpwapwa kutokana na  kuviharibu wenyewe.

Nao baadhi ya wakazi wa vijiji hivyo wamesema kuwa uharbifu huo umekuwa ukichangia  kwa kiasi kikubwa changamoto ya ukosefu wa maji kuwa kubwa katika maeneo yao na wameiomba serikali kulitazama jambo hilo kwa jicho la tatu ikiwa ni pamoja na kutoa elimu ya utunzaji wa mazingira kwa jamii.

NAALFREDBULAHYA                                               DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...