Skip to main content

TFS INATARAJIA KUPUNGUZA MATUMIZI YA NISHATI YA MKAA NA KUNI NCHINI

                                   
                Image result for MAMLAKA YA HUDUMA ZA MISITU TFS


Waziri wa Maliasili na Utalii Dk, Hamisi Kigwangala  ameliagiza  baraza la wafanyakazi  na wakala wa huduma za misitu Nchini TFS kushirikiana kwa pamoja  kusimamia kikamilifu Rasiliamali za misitu ili kudhibiti Uharibifu unao tokana na shughuli za kibinadamu.

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo katika uzinduzi wa Baraza la wafanyakazi na wakala wa huduma za misitu TFS DK KIGWANGALA  Amesema ili kudhibiti uharibifu wa rasiliamali hizo baraza linatakiwa kutoa  mapendekezo na mikakati  ya namna ya kudhibiti uharibifu huo.

DK KIGWANGALA ameongeza kuwa uchomaji  mkaa, uvunaji wa mbao pamoja na shughuli za kilimo imekuwa ni vyanzo vikuu vinavyopelekea uharibifu wa misitu hapa nchini.

Katika hatua nyingine DK KIGWANGALA amesema asilimia 95 ya mikoa yote nchini  wananchi wanatumia nishati ya mkaa pamoja na kuni na kupelekea kiasi kikubwa cha utoroshwaji wa nishati hiyo kwenda nchi jirani ikiwepo nchi ya  Kenya na Sudani kusini.

Kwa upande waka Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya huduma za misitu Tanzania Prof ,DOS SANTOS SILAYO amesema ili kukabiliana na uharibifu wa misitu wanatarajia kupunguza matumizi  ya nishati ya mkaa   pamoja na kuchukua hatua kwa wanaofanya uharibifu wa rasiliamali za misitu.

Na Mindi Joseph, Mabawa                             Chanzo Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...