Skip to main content

TAKWIMU ZINAONESHA JAN – MARCH 2018 JUMLA YA WAHAMIAJI HARAMU 103 WAMEKAMATWA MJINI DODOMA.

Wakazi mkoani Dodoma wametakiwa kushirikiana na idara ya uhamiaji pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama kwa kutoa taarifa  za wahamiaji haramu na kuacha kuwahifadhi nyumbani watu wasiowajua ili kusaidia kudhibiti wahamiaji haramu kuingia na kukaa nchini.


Akizungumza na Dodoma FM mapema leo Afisa Uhamiaji wa Mkoa wa Dodoma PETER J KUNDY amesema Jukumu la idara ya uhamiaji ni kuhakikisha linafanya usimamizi na udhibiti wa mipaka ya nchi ,utoaji wa hati za kusafiria kwa raia na hati za makazi kwa wahamiaji na wananchi wanatakiwa kushirikiana na idara hiyo ili kusaidia kudhibiti wahamiaji hao.

Bwana KUNDY amebainisha kwa  mwaka 2017  idara ya uhamiaji kwa kutumia Doria,misako na kaguzi  wamefanikiwa kukamata wahamiji haramu 70 Raia wa nchi za Ethiopia,Bururndi,China,Kongo,Kenya,India pamoja na Malawi na kuchukuliwa hatua mbalimbali.

Katika hatua nyingine ameongeza kuwa wamiliki wa vyombo vya usafiri wanatakiwa kuhakikisha vyombo vyao vya usafiri havitumiki kusafirisha wahamiaji haramu pamoja na wamiliki wa shule binafisi kuhakikisha waalimu na raia wa kigeni watakao waajiri wana vibali kutoka idara ya uhamiaji na wizara ya kazi.

Takwimu zinaonesha kwa mwaka 2018 kuanzia January hadi march watuhumiwa waliokamatwa ofisi ya uhamiaji mkoa wa Dodoma jumla ni 103 huku Ethiopia ikiongoza kwa wahamija haramu kuingia nchini.

Na,Mindi Joseph,Hadija                                   Chanzo: Dodoma   FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...