Skip to main content

TAASISI MBALIMBALI ZASISITIZWA KUZINGATIA KANUNI ZA USALAMA KAZINI.


      Image result for usalama mahala pa kazi


Wakala wa usalama na afya mahala pa kazi nchini (OSHA) iliyopo chini ya waziri wa kazi,vijana, ajira na watu wenye ulemavu wamezitaka sekata mbalimbali kuzingatia sheria kanuni na taratibu za usalama na afya mahala pa kazi wakati wakiendesha shughuli zao.

Kauli hiyo imetolewa mjini Dodoma na mkaguzi wa ujenzi kutoka OSHA kanda ya kati Mhandisi Robert Mashinji wakati akizungumza na Dodoma FM kuelekea maadhimisho ya kila mwaka ya siku ya usalama na afya mahala pa kazi yanayotarajia kufanyika kitaifa mkoani Iringa ifikapo april 28 mwaka huu.

Mashinji amesema taasisi na wadau mbalimbali wanaojihusisha na utoaji wa huduma mbalimbali kwa jamii kama  vituo vya kuuza mafuta, kumbi za starehe na zile za mikutano zinapaswa kutambua matumizi sahihi ya vifaa kinga mahala pa kazi ikiwemo kuweka vifaa vya kudhibiti hatari kama majanga ya moto katika maeneo yao ya kazi.

Ameongeza kuwa osha imekuwa ikifanya kazi ya ukaguzi katika maeneo yenye mikusanyiko ya watu kama viwanda,migodi, miradi ya ujenzi,  benki, hospitali pamoja na nyumba za kulala wageni  ili kuangalia namna waajiri wanavyowakinga wafanyakazi dhidi ya vihatarishi mahala pao pa kazi na inapobaini kuwepo kwa ukiukwaji hatua kali huchukulia ikiwemo adhabu za papo kwa papo au kufikishwa mahakamani.

Aidha bwana Mashinji amewakumbusha wadau kwa kutaja vifaa vinavyokaguliwa kuwa ni pamoja na usalama wa mtandao wa umeme, miundombinu ya kujiokoa wakati wa dharura, ubora wa mazingira ya kufanyia kazi pamoja na usahihi wa vifaa kinga anayopewa mfanyakazi.

Maadhimisho ya siku ya usalama na afya mahala pa kazi huadhimishwa duniani kote kila mwaka ifikapo april 28 na kwa mwaka huu nchini Tanzania yataadhimishwa kitaifa mkoani Iringa yakiwa na kauli mbiu isemayo "kizazi salama chenye afya kwa maendeleo ya viwanda".

Na Alfred Bulahya                                                     Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...