Skip to main content

SHEREHE ZA MUUNGANO KITAIFA KUFANYIKA MKOANI DOODOMA MGENI RASMI RAIS MAGUFULI


Image result for SHEREHE ZA MUUNGANO DODOMA


Katika kuelekea kwenye maadhimisho ya  miaka 54 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar imeelezwa kuwa  licha ya kuwepo kwa mafanikio ya kisiasa pia mwananchi mmoja mmoja anafaidika katika kuinuka kiuchumi pamoja na kupata nafasi ya kumiliki ardhi katika pande zote mbili.

Kaimu mkurugenzi Idara ya Muungano Ofisi ya Makamu wa Rais  Bw,Sifuni Joshua Msangi amesema muungano umesababisha wananchi kunufaika kwa kumiliki ardhi na kufanya shughuri za kilimo na uwekezaji pamoja na utaliii kwa wananchi wa  Tanzania bara pamoja na Zanzibar.

Amesema serikali ya jamuhuri ya muungano wa Tanzania imekuwa ikifanya shughuri nyingi katika kuwawezesha wananchi wa pande zote mbili kushiriki katika shughuri za uzalishaji zinazowawezesha wananchi kuinuka kiuchumi ikiwemo katika miradi ya kilimo.

Kwa upande wao baadhi ya Wananchi wamesema kuwa muungano umekuwa na faida nyingi katika maisha yao ya kila siku ikiwemo kuimarisha ulinzi na usalama katika jamii, kuwepo kwa amani na upendo katika pande zote mbili.

Maadimisho ya miaka 54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar  yanatarajiwa kuadhimishwa mkoani hapa  huku kauli mbiu ikiwa ni MUUNGANO WETU NIWAMFANO DUNIANI TUUENZI, TUULINDE, TUIMARISHE NAKUUDUMISHA KWA MAENDELEO YA TAIFA LETU

Na Phina Nimrod                                     Chanzo:Dodoma Fm

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...