Skip to main content

SERIKALI YAZINDUA MFUMO MPYA WA HATI ZA KUSAFIRIA ZA KISASA

             Image result for WAZIRI MWIGULU AZINDUA PASSPORT



Serikali kupitia wizara ya mambo ya ndani ya nchi imezindua rasmi mfumo wa utoaji hati za kisasa za kusafiria kwa njia ya kielectroniki ikiwa ni miongoni mwa hatua za kuendelea kupunguza uhalifu unaofanywa na watu mbalimbali wakiwemo wahamiaji haramu hapa nchini.

Zoezi hilo limezinduliwa mapema hii leo Jijini Dodoma na waziri wa mambo ya ndani Mwigulu Nchemba na kuwataka wananchi watakaopatiwa hati hizo kuhakikisha wanatunza kikamilifu ili kuepusha kutumiwa na wahalifu mbalimbali.

Amesem kuwa ni vyema wananchi wakatambua umuhimu wa kuwa na hati hizo ili kuepusha usumbufu unaoweza kujitokeza kama kuhusishwa na mambo ya kihalifu kwani  kuna baadhi ya watu ambao hupata pasipoti kwa njia ya mkato na kwenda kuzifanyia uhalifu katika nchi za nje kitu ambacho kinaidhalilisha Tanzania.

Pamoja na hayo amesema, uzinduzi huo una lenga kukidhi matakwa ya usalama wa nchi na viwango vya kimataifa na kwamba pasipoti hizi zimetengenezwa kwa teknolojia ya kisasa  na zitakuwa na uwezo wa kubeba taarifa za mwombaji bila kugushi na amesema pasipoti za zamani zitaendelea kutumika hadi mwezi January mwaka 2020 .

Kwa upande wake kamishina Jenerali wa uhamiaji Dkt.Anna Peter amesema kuwa pasipoti hizo zitatumika kwa kipindi cha miaka kumi ambapo gharama yake ni sh.laki moja na nusu serikali ina mpango mkakati wa kueneza zoezi hili nchi nzima ili kuwafikia wananchi wote na kwamba kila atakayekuwa na pasipoti atakuwa na nakala ya pasipoti hiyo kwenye simu yake ya kiganjani.

Sambamba na hayo ametaja idadi ya pasipoti ambazo zimekwisha kutolewa kwa wananchi tangu Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania azindue zoeli hili mwezi January mwaka huu jijini Dar es Salaam kuwa ni 10863.

Na Alfred Bulahya                                                               Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...