Skip to main content

SERIKALI YATOA MAJIBU YA KUTOONEKANA KWA TRILIONI 1.5 KATIKA RIPOTI YA CAG

          Image result for DR ASHATU KIJAJI BUNGENI             
                         


Serikali kupitia wizara ya fedha na mipango imetolea ufafanuzi juu ya hoja ya kuto kuonekana kwa matumizi ya Serikali ya kiasi cha Trilioni 1.51 kutokana na ripoti ya mkaguzi na mdhibiti mkuu wa hesabu za Serikali (CAG).

Naibu Waziri wa fedha na mipango Dr. Ashantu Kijaji ametoa ufafanuzi huo leo Bungeni mjini Dodoma wakati akitoa kauli rasmi ya Serikali juu ya fedha kiasi cha trilioni 1.51 zinazodaiwa kuto kuonekana matumizi yake.

Amesema katika kipindi cha mwaka 2012/13 hadi 2016/17 Serikali kupitia Wizara ya fedha ilikuwa katika kipindi cha mpito cha miaka mitano ya mpango mkakati wa kuandaa hesabu za Serikali kwa kutumia mfumo wa viwango vya kimataifa vya uhasibu katika sekta ya umma.

   Naibu Waziri Dr. Ashantu Kijaji amesema katika taarifa ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za Serikali CAG imeeleza jumla ya mapato ya Serikali kwa mwaka 2016/17 yalikuwa trilioni 25.3 fedha hizo zikijumuisha mapato ya kodi, mapato yasiyo ya kodi mikopo ya ndani na nje ikiwemo misaadsa  na mikopo nafuu kutoka kwa washirika wa maendeleo.


Ufafanuzi huo unakuja ikiwa ni siku chache baada ya mwenyekiti wa chama cha ACT Wazalendo Mh. Zitto Kabwe alizungumza na vyombo vya habari na kueleza kuwa katika ukurasa wa 34 wa ripoti ya mkaguzi  na mdhibiti mkuu wa hesabu za Serikali CAG kunaonesha kiasi cha sh. Trilioni 1.51 hazikutolewa kwa matumizi wala kukaguliwa.

Na Pius Jayunga                                              Chanzo: Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...