Skip to main content

SERIKALI YADHAMIRIA KUENDELEA KUBORESHA UFUNDISHAJI WA MASOMO YA SAYANSI

        Image result for Ester Bulaya bungeni

Serikali imedhamiria kuendelea kuboresha ufundishaji wa masomo ya sayansi  ili kuongeza idadi ya wasomi waliobobea katika masomo ya sayansi.


Naibu Waziri wa elimu sayansi na teknolojia Mh. Tate Ole Nasha ameyasema hayo leo Bungeni Mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa jimbo la Bunda  Mjini Ester Bulaya alietaka kufahamu ni kwa kiasi gani tatizo la upungufu wa walimu wa masomo ya sayansi limeweza kutatuliwa.

Amesema Serikali imekwisha kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kuimarisha ufundishaji wa masomo ya sayansi na hisabati, ambapo wahitimu 1799 wa kundi la kwanza watahitimu masomo yao ifikapo mwezi wa 5, 2018 kundi la pili likiwa na wahitimu 5401 ambao wanatarajiwa kuhitimu ifikipo mei, 2019.

Hata hivyo Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini Ester Bulaya amesema katika Jimbo lake kuna uhaba mkubwa wa walimu wa masomo ya sayansi hatua inayochangia wanafunzi katika Wilaya hiyo kufanya vibaya katika masomo yao huku Naibu Waziri wa elimu Mh. Tate Ole Nasha akisema changamoto hiyo ni  kwa Nchi nzima .

Katika hatua nyingine Naibu Waziri Tate Ole Nasha amesema Serikali haitarajii kuwarudisha shuleni wanafunzi waliobebeshwa ujauzito wakiwa shuleni na kwamba kufanya hivyo ni sawa na kuhamasisha vitendo vya ngono kwa wanafunzi na hii ni kufuatia  swali la Mbunge Rehema Migige aliehoji ni lini Serikali itawarejesha masomoni wanafunzi walio bebeshwa ujauzito.

Na PIUS JAYUNGA                                                           DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...