Skip to main content

RAISI AMPA MAAGIZO MAZITO RC DODOMA KUFUATIA UBADHIRIFU WA FEDHA ZA MAJI

                 Image result for JIJI LA DODOMA


Rais John Magufuli amemtaka Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Isaac Kamwelwe na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge kufuatilia ubadhirifu wa fedha za mradi wa maji katika Mkoa wa Dodoma na kuhakikisha wahusika wanakamatwa au maji yanatoka.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Aprili 27, wilayani Kondoa wakati wa hafla ya uzinduzi wa barabara ya Dodoma – Babati yenye urefu wa kilomita 251 ambayo ni sehemu ya barabara kuu inayotoka Capetown, Afrika Kusini mpaka Cairo, Misri.

Ameagiza vyombo vya dola kuwatafuta wahusika wa ubadhirifu wa fedha hizo ambazo amesema ni zaidi ya Sh2 bilioni.

Amesema ni lazima wahusika wachukuliwe hatua kwa sababu hizo ni fedha za wananchi, na ni vyema ziwaletee maendeleo.

“Haiwezekani tukawa tunaimba maji kila siku halafu maji hayatoki. Vyombo vya dola vihakikishe wahusika wote wanakamatwa au maji yanatoka. Tukibembelezana hivi hatutafika, hata hii barabara tusingebana, isingekamilika,” amesema Rais Magufuli.

Awali kabla ya Rais Magufuli kuzungumza, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge alisema kuna ubadhirifu wa Sh1.5 bilioni kwenye mradi wa maji katika wilaya za Kondoa na Chemba ambao mpaka sasa  unasuasua.

Mkuu huyo wa mkoa alisema mradi huo ulitengewa  Sh2.8 bilioni kwa ajili ya wilaya hizo, lakini kulitokea ubadhirifu wa Sh1.5 bilioni.

Amebainisha kwamba vyombo vya dola vinaendelea na uchunguzi wa ubadhirifu huo.

Na Zania Miraji                                                                     Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...