Skip to main content

RAIS MAGUFULI ATAKA WANAOTOA TAKWIMU ZA KUPOTOSHA MITANDAONI WASHUGHULIKIWE

           Image result for RAIS MAGUFULI IKULU



Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli amewataka wanasheria Nchini kusimamia ipasavyo sheria za nchi katika kudhibiti vitendo vya baadhi ya watu wanaotumia mitandao ya kijamii kwa kutoa takwimu za kupotosha umma.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo Ikulu Jijini Dar Es Salaam wakati akiwaapisha majaji 10 Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka pamoja na Naibu Wakili wa Serikali walioteuliwa na Rais Magufuli hivi karibuni.

Rais Magufuli amewataka wanasheria pamoja na majaji kuzishughulikia mapema kesi za watu wanaotuhumiwa kujihusisha na utoaji wa taarifa za uongo katika mitandao ya kijamii na hatimae kupotosha umma wa watanzania juu ya taarifa rasmi zinazotolewa na Serikali.

Kwa upande wake waziri wa katiba na sheria prof. Paramagamba Kabudi amesema katika kipindi hiki kesi nyingi zimeibuka na hii ni kutokana na nchi za Afrika zinapochukua maamuzi ya kufanya maendeleo kwa wananchi hujuma nazo huongezeka ili kukwamisha jitihada hizo.

Akifafanua utaratibu wa kuchanguliwa kwa majaji hapa nchini Jaji mkuu wa tanzania Prof. Ibrahimu Hamis Juma amesema ili kuondoa hujuma na taarifa za upotoshaji mitandaoni tume hutoa nafasi kwa wadau wa sheria kutoa majina ya watu wanaoweza kukidhi matakwa ya katiba na walio na uwezo wa kufanya shughuli za ujaji.

Na Pius Jayunga                                          Chanzo: Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...