Skip to main content

RAIS MAGUFULI AMERASIMISHA MKOA WA DODOMA KUWA JIJI


Image result for rais Magufuli muungano

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli leo ametangaza rasmi kuupa hadhi ya Jiji Mkoa wa Dodoma kutoka ngazi ya Manispaa.

Rais Magufuli ametangaza uamzi huo wakati akihutubia wananchi katika maadhimisho ya miaka 54 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar maadhimisho yaliyofanyika katika uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma.

Wakati huo huo aliekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma Bw. Godwin Kunambi amepandishwa hadhi na kuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma.

Rais Magufuli amesema azma ya Serikali kuhamia makao makuu ya Nchi Dodoma haitarudi nyuma na tayari watumishi zaidi ya 3800 wameshahamia Dodoma ambapo ameagiza maandalizi yote ya kisheria kufanyika mapema.


Mh Magufuli amewahakikisha watanzania kuwa Serikali ya awamu ya tano itaendelea kuuenzi muungano na kuwataka wananchi kudumisha upendo, umoja na mshikamano huku akieleza baadhi ya mambo yaliyofanikiwa katika Serikali ya awamu ya tano kuwa ni pamoja na kukua uchumi kwa asilimia 7 na kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa malaria kutoka asilimia 14.3 hadi asilimia 7.3%.

Baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Dodoma wakizungumza na Dodoma FM kwa nyakati tofauti wamesema Muungano wa Tanganyika na Zanzbar umeleta mafanikio makubwa Nchini hasa katika kudumisha amani, upendo, mshikimano sambamba na viongozi wakiwemo wananchi kila mmoja kuwajibika kwa nafasi yake ili kuleta maendeleo Nchini.

Maadhimisho ya sherehe za muungano wa Tanganyika na Zanzibar yamefanyika leo hapa Jijini Dodoma mgeni rasmi akiwa Rais na amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama Nchi Rais Dr. John Pombe Magufuli huku maadhimisho hayo yakibebwa na kaulimbiu isemayo miaka 54 ya Muungano wetu ni mfano wa kuigwa Duniani, tuuenzi, tuulinde na kuudumisha kwa maendeleo ya Taifa letu.

Na Pius Jayunga                                                                      Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...