Skip to main content

RAIS DKT MAGUFULI AZINDUA MRADI WA KUZALISHA UMEME WA KINYEREZI ll JIJINI DAR ES SALAAM LEO

                 Image result for RAIS AZINDUA MRADI WA UMEME KINYEREZI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli amesema licha ya kupiga hatua katika uzalishaji wa nishati ya umeme nchini bado wananchi wanalazimika kutumia nishati ya mkaa, kuni na mafuta ya taa.

Rais Magufuli ameyasema hayo leo wakati akizindua Mtambo wa Kufua Umeme wa Kinyerezi II uliopo katika jimbo la segerea Jijini Dar es salaam na kueleza kuwa kuna haja ya kuendelea kuzalisha nishati ya umeme zaidi ili kutosheleza mahitaji ya watanzania.

Amesema kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na ofisi ya takwimu kwa mwaka 2015/16 inaonesha asilimia 36.6 ya watanzania ndio waliounganishwa na huduma ya nishati ya umeme na waliobaki wakiwa wanatumia nishati ya mkaa, kuni pamoja na mafuta katika matumizi yao.

Rais Magufuli amesema kutokana na matumzi ya nishati ya kuni na mkaa yamechangia kwa kiasi kikubwa uharibifu wa mazingira ambapo kila mwaka hekta 400 elfu za misitu zinaharibiwa kutokana na ukatiji wa miti pamoja na madhara ya kiafya hivyo ni lazima uzalishaji wa nishati ya umeme uendane sambamba na mahitaji ya idadi ya watanzania.

Nae Waziri wa nishati Dr. Medard Kaleman amesema katika kipindi cha miaka mitatu ijayo eneo la kinyerezi litakuwa na uwezo wa kuzalisha umeme mega wati 1692 kutokana na jitihada zinaendelea kufanyika katika kukamilisha miradi iliyosalia.

Mradi wa kufua umeme wa kinyerezi II uliozinduliwa leo na Rais Dr. John Pombe Magufuli unatarajiwa kuzalisha umeme wa mega watt 240.

Na Pius Jayunga                                                        Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...