Skip to main content

MIKAKATI YA SERIKALI KATIKA KUPUNGUZA VIFO VYA MAMA NA MTOTO

  Image result for DR FAUSTINE NDUGULILE                   



Naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dr. Faustine Ndugulile amesema Serikali inatambua kuwepo kwa ongezeko la vifo vya mama na mtoto huku ikiendelea na mikakati mbalimbali inayolenga kupunguza vifo hivyo.

Dr. Ndugulile ametoa kauli hiyo leo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge Halima Abdalha Bulembo alietaka kufahamu Serikali ina mkakati gani kupunguza vifo vya mama pamoja na watoto hasa kwa watoto njiti.

Amesema mkakati unaondelea kwa sasa ni pamoja na kuboresha vituo vya afya Nchini katika vituo vya dharula, kuweka mkakati wa huduma za watoto njiti na watoto waliozaliwa katika kipindi maalumu, zinapatikana katika hospitali zote zikiwemo hospitali za Wilaya, Mkoa na Rufaa.

Kwa upande wake Naibu waziri wa Tamisem Mh. Joseph Sinkamba Kandege amesema Wizara imetenga kiasi cha shilingi mil. 22.1 kwa mwaka wa fedha 2018/19 kwa ajili ya kutolea mafunzo maalumu ya kumsaidia mtoto njiti na hadi sasa kumekuwepo na mashine za aina tatu zinazo weza kuwasaidia watoto wachanga kupumua.

Kwa mjibu wa ripoti iliyochapishwa mwaka 2012 na jopo la wataalamu wa wakilishi wa mashirika ya umoja wa Mataifa, Nchini Tanzania takwimu zinaonesha asilimia 13 ya watoto huzaliwa wakiwa na uzito pungufu ambao huchangia kwa asilimia 86 ya vifo vya watoto wachanga.

Na Pius Jayunga                                                            Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...