Skip to main content

MAVUNDE AMEAHIDI KUTATUA CHANGAMOTO KATIKA SHULE YA SEKONDARI DODOMA

                                          Image result for Antony Mavunde Mahafali dodoma sekondari                                                             


Wahitimu wa kidato cha sita katika shule ya sekondari Dodoma wametakiwa kuhakikisha wanaitumia vizuri elimu waliyoipata kwa kuwa mabalozi wakubwa katika kusaidia ujenzi na ustawi wa taifa ili kuleta mabadiliko chanya katika jamii.

Kauli hiyo imetolewa leo na Naibu Waziri wa Kazi, Vijana na Ajira, ambae pia ni mbunge wa jimbo la Dodoma Mjini Mhe. Anthony Mavunde wakati akitoa hotuba kwa wanafunzi wa shule ya sekondari Dodoma  katika mahafali ya 15 ya kidato cha sita.

Mavunde Amesema kuwa wahitimu hao wanatakiwa kuwa mabalozi wazuri kwenye jamii katika kutoa elimu juu ya maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi pamoja na madhara ya matumizi ya madawa ya kulevya ambayo yamekuwa yakichangia kuongeza kundi kubwa la watu wenye utegemezi.

Awali akisoma risala mbele ya mgeni rasimi mkuu wa shule ya sekondari Dodoma AMANI MFAUME ameiomba serikali kuhakikisha inatatua changamoto ya upungufu wa mabweni kwa ajili ya wanafunzi wa kiume kwani jambo hilo limekuwa likisababisha baadhi ya wanafunzi kupanga vyumba mitaani hali ambayo inawafanya kukosa usimamizi katika masomo na kusababisha kuwa na ushiriki hafifu kwenye masomo yao.

Amesema mbali na hilo baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakijikuta wakiingia katika vishawishi mbalimbali vya kuishi katika maisha ya kimjini na kusababisha matokeo yao kuwa mabaya ukilinganisha na upande wa wasichana ambao wanaishi ndani ya eneo la shule.

Naibu waziri  Mavunde ameahidi kuhakikisha changamoto hizo zinatatuliwa katika shule hiyo ili kuwajengea uwezo mkubwa wa kitaaluma wanafunzi hao.

Na Alfred bulahya                                                            Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...