Skip to main content

MAPAMBANO DAWA ZA KULEVYA WAFANYABIASHARA 3486 WAMEFIKISHWA MAHAKAMANI

Image result for NAIBU WAZIRI WA AJIRA ANTONY MAVUNDE
                               

Serikal imesema itaendelea kuhakikisha inapambana na kila aina ya mianya inayotumika katika kusafirisha dawa za kulevya wakiwemo pia watumiaji wa dawa hizo.

Naibu Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri mkuu kazi vijana na ajira Mh. Anthony Mavunde ameyasema hayo leo Bungeni Mjini Dodoma wakati akitolea ufafanuzi hatua zinazochukuliwa na Serikali ili kukabiliana na wale wanaoendelea na biashara hiyo.

Mh. Mavunde amesema hadi kufikia mwezi february mwaka 2018 jumla ya wafanyabiashara 3486 wa dawa za kulevya wamekwisha kufikishwa mahakamani na kati ya hao zaidi ya asilimia 30 ni wafanyabiashara wakubwa.

Naibu Waziri Mavunde amesema Serikali imejitahidi kutoa elimu kwa waathirika wa matumzi ya dawa za kulevya na hadi kufikia mwezi february 2018 waraibu wapatao 5560 wameendelea kupata tiba katika vituo 5 vya Serikali na lengo ikiwa ni kusambaza huduma hiyo Nchi nzima ili kuwafikia waraibu wengi zaidi.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi ofisi ya Waziri mkuu sera, bunge, kazi vijana na wenye ulemavu Mh. Jenista Mhagama amewataka wamiliki wa soba house Nchi nzima kuacha mara moja kuwaweka vijana katika kambi hizo kwa faida binafisi bila msaada maalumu.

Na Pius Jayunga                                                                Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...