Skip to main content

MAASKOFU WAONYWA KUINGILIA SIASA NA KUTAKIWA KUTATUA MIGOGORO NCHINI

                                    Image result for ASKOFU DAMASI MUKASSA


Maaskofu na watumishi  wa dini nchini wameshauriwa kuacha kuingia kwenye masuala ya kisiasa yanayochochea kuleta malumbano kwa jamii na badala yake wajikite  kutatua migogoro iliyopo nchini.

Ushauri huo umetolewa leo na askofu mkuu wa makanisa ya pentekoste mjini Dodoma ambaye pia ni mwenyekiti wa umoja wa madhehebu ya kikirsto mkoa wa Dodoma askofu Damas Mukassa wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa.

Amesema kuwa nchi ya Tanzania bado ina changamoto nyingi zinazopaswa kushughulikiwa hivyo ni vyema watumishi wote wa dini wakaachana na mambo yanayokinzana na shughuli zinazochangia kuleta maendeleo kwa jamii bali  waunge mkono juhudi zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano ili kuendelea kukuza uchumi wa nchi na hasa uchumi wa viwanda.

Askofu Mukassa amewataka pia kuacha kulalamikia ugumu wa maisha wakidai serikali imebana pesa bali wafanye kazi mbalimbali zinazoweza kuwaingizia vipato pamoja na kutekeleza majukumu yao waliyopewa na taasisi zao kama kukemea masuala ya uovu na ufisadi .

Katika hatua nyingine askofu Damas amelaani na kupinga vikali taarifa zinazosambazwa mitandaoni za kutaka wananchi wanafanye maandamano mnamo april 26 mwaka huu kwani madai yanayodaiwa hayana tija kwa taifa ambapo amewaomba wananchi kupuuza taarifa hizo huku pia akiviomba vyombo vya dola kusimama imara ili kuhakikisha jambo hilo halitokei.

Na Alfred Bulahya                                                            Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...