Skip to main content

KIWANGO CHA MAAMBUKIZI YA UGONJWA WA MALARIA KIMESHUKA HADI KUFIKIA ASILIMIA 7.3

                           Image result for MAADHIMISHO YA MALARIA



Kiwango cha maambukizi ya ugonjwa wa Malaria  nchini  kimeshuka kwa nusu zaidi kutoka asilimia 14.4 mwaka 2015 hadi kufikia asilimia 7.3 mwaka 2017.

Hayo yamebainishwa Leo na Waziri wa Afya maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto  Mh. Ummy Mwalimu wakati wa maadhimisho ya siku ya malaria Duniani ambayo kwa Tanzania Kitaifa yamefanyika  Wilayani Kasulu Mkoani Kigoma.

Waziri UMMY amesema kuwa ili watanzania tuendelee kutokomeza  ugonjwa wa malaria watanzania wanatakiwa kushiriki kikamilifu katika kutumia afua zote za kupambana na ugonjwa huo ikiwemo kunyunyizia viuadudu vya kuua viluilui vinavyoweza kuleta malaria.

Vilevile waziri Ummy amesisitiza kuwa kila halmashauri za kila wilaya kuunda kamati zitakazo hamasisha usafi wa mazingira  ili kuondoa mazalia ya mbu katika kutokomeza malaria

Sambamba na hilo Mh.UMMY amezindua takwimu za ugonjwa wa malaria nchini ambao umefanywa na Taasisi ya takwimu NBS ambayo ndiyo  takwimu itakayotumiwa na serikali ya Tanzania

Kwa upande wake waziri wa elimu na ufundi Prof Joyce Ndalichako amesema kuwa atahakikisha  wanafunzi wanapambana na ugonjwa wa malaria kwa kuweka somo la afya kwa shule zote za msingi na sekondari nchini.

Kilele cha maadhimisho ya siku ya Malaria Duniani kimefika tamati leo  kwa kufanyika  katika wilaya ya Kasulu Mkoani KIGOMA ikiwa yamebeba  kauli mbiu isemayo NIPO TAYARI KUTOKOMEZA MALARIA WEWE JE..?

NA LUCAS GODWIN                                      CHANZO :WIZARA YA AFYA

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...