Skip to main content

KWA MWAKA MMOJA WATU ZAIDI YA ELFU 11 WAMEKAMATWA KWA TUHUMA ZA DAWA ZA KULEVYA NA

                                              Image result for WAZIRI ANTONY MAVUNDE

Kufuatia kutungwa kwa sheria mpya namba 5 ya mwaka 2015  ya kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya nchini imechangia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa kasi ya mapambano ya kudhibiti dawa hizo.

Naibu waziri wa ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira na watu wenye ulemavu Mh. Athony Mavunde ameyasema hayo leo Bungeni Mjini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu Mwantumu Dau Haji aliehoji ni hatua zipi zimechukuliwa katika mapambano ya kudhidhiti biashara ya dawa za kulevya.

Mh. Mavunde amesema sheria hiyo imeipa Serikali mamlaka makubwa ya kuanzisha chombo cha kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya kilichoundwa mwaka 2017 kikiwa na mamlaka ya kukamata, kupekua, kuzuia mali na kuchunguza mashauri yote ya dawa za kulevya.

Amesema katika kuongeza kasi dhidi ya mapambano ya dawa za kulevya mwaka, 2017 yalifanyika marekebisho madogo katika sheria hiyo na kuipa mamlaka mara dufu ambapo katika kipindi cha mwaka mmoja hadi kufikia February 2018 watuhumiwa 11,071 walikamatwa wakiwemo watuhumiwa 3486 ambao ni wafanyabiashara wa dawa za kulevya.

Awali Naibu Spika Mh. Tulia Ackson, ameongoza zoezi la kuwaapisha wabunge wawili, Dk Godwin Mollel wa jimbo la Siha na mbunge Maulid Mtulia wa jimbo la Kinondoni baada ya kufanyika kwa uchaguzi mdogo katika majimbo hayo kufuatia wabunge wa maeneo hayo kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Na Pius Jayunga                                                                  Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...