Skip to main content

JUWACHA WAOMBA SERIKALI IONGEZE JITIHADA KATIKA SEKTA YA AFYA CHANGAMOTO BADO NI NYINGI

           Image result for JUKWAA LA WAKULIMA WANAWAKE


ukwaa la wakulima la wanawake Wilaya ya Chamwino (JUWACHA) lililopo chini ya shirika lisilo la kiserikali la Action Aid limeiomba serikali  kuongeza jitihada katika sekta ya afya kutokana na zahanati ya Mlodaa kukabiliwa na upungufu wa wahudumu,madaktari, pamoja na dawa. 

Hayo yamebainishwa na mwenyekiti wa Jukwaa hilo Bi. Janeth Nyamayahasi wakati akiwasilisha taarifa ya matokeo ya tathmini ya pima kadi kuhusu huduma za jamii.

Amesema sekta ya afya inakabiliwa na changamoto ikiwa ni pamoja na upungufu wa zahanati katika kata mbalimbali na nyingine kukabiliwa na upungufu wa wahudumu, madaktari, pamoja na dawa  hali inayopelekea jamii kutopata matibabu kwa ubora.
Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Chamwino Andrew Kayamgoya amesema ni kweli matatizo hayo yapo ikiwemo uhaba wa watumishi kwenye idara ya afya unaochangiwa na kustaafu kwa baadhi ya watumishi , pamoja na kuhamishiwa sehemu nyingine.
Matokeo ya tathmini hiyo yamefanyika Katika kata nane za wilaya ya Chamwino ikiwemo Mlowa Barabarani, Iringa Mvumi, Makang’wa, Buigiri, Chamwino, Msanga,Chilonwa Na Machali ambayo yamefanywa na Jukwaa la wakulima wanawake wilayani hapo JUWACHA lililopo chini ya shirika lisilo la kiserikali la ACTION AID.

Na,Mindi Joseph                                                                 Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...