Skip to main content

JESHI LA POLISI DODOMA LINASHIKILIA WAHAMIAJI HARAMU SABA

                                         Image result for JESHI LA POLIS DODOMA LAKAMATA WAHAMIAJI HARAMU   


Jeshi la polisi mkoa wa Dodoma limewakamata wahamiaji haramu saba ambao sita kati yao ni wasomali wenye uraia wa Kenya walioingia nchini Tanzania bila kibali halali.

Akizungumza na waandishi wa habari mapema hii leo Kamanda wa polisi mkoani hapa GILLES MUROTO amesema Uchunguzi wa awali unaonekana wahamiaji hao  wanaingia nchini kupitia mpaka wa Namanga-ARUSHA na hati zao zimegongwa mihuri inayo tofautiana na kutiliwa mashaka kuwa sio hati halali.

Kamanda MUROTO amewataja wahamiaji haramu kuwa ni Mussa Abdi Isaka mwenye umri wa miaka 37, Aden Awes Abdi 34, John Gichuchi Mbogo 28,Abraham Hussein Ismail 22, Joseph Mbuthia Kibuko 33,Mohamed Abdi Kosar 28  wote wakiwa ni Raia wa kenya wamekamatwa kwenye basi la kampuni ya NGASERE lenye namba T.675 DJT linalofanya safari zake kati ya Mpwapwa na Iringa.

Wakati huo huo Jeshi la polisi limefanikiwa kukamata watu wawili ambao ni wavunjaji wa nyumba na kuiba mali mbalimbali za wizi ambazo ni Laptop 2 aina ya lenovo na Sony , Desktop computer 1 aina ya Dell, Flat screen TV aina ya Samsung watuhumiwa hao wakiwa ni Beda Nathaniel 31 , Dickson Mrisho 27 wanaofanya kazi ya ujenzi na ni wakazi wa Makuru Dodoma.

Kamanda MUROTO amesema wahalifu wengi wa uvunjaji ni mafundi ujenzi hivyo ametoa tahadhari kwa wananchi wa Dodoma kuchukua tahadhari ya mafundi kwa kuwa ndio wanaorudi kuvunja na kuiba baada ya kujenga wenyewe.

Sambamba na hayo Jeshi la polisi linawapongeza watoa Taarifa kwa kutambua uhalifu na kuchukua hatua mapema kwa kutoa Taarifa kwa jeshi la polisi na kuwataka wamiliki na wafanyakazi katika vyombo vya Usafiri wasikubali kuingia matatizoni kwa kusafirisha wahamiaji haramu kwa kuwa magari yao yatataifishwa kwa mujibu wa sheria.

Na ANIPHA RAMADHAN                                   DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...