Skip to main content

ASILIMIA 37 YA WATOTO HUZALIWA NA MATATIZO YA UTINDIO WA AKILI,MGONGO WAZI NA VICHWA VIKUBWA MJINI DODOMA

Baadhi ya mikoa nchini  Tanzania imegundulika kuwa na changamoto ya kuzaliwa kwa watoto wenye mtindio wa akili,mgongo wazi, pamoja na kuzaliwa na vichwa vikubwa na hii ni kutokana na kinamama wajawazito kutozingatia mlo kamili wawapo katika kipindi cha ujauzito.


Hayo yamebainishwa na Afisa lishe Mkoa wa Dodoma Bi.Mariam Mwita wakati akizungumza na Dodoma FM ambapo amewataka kinamama wajawazito kuwekeza katika siku elfu moja (1000)tangu mimba inapotungwa,Mtoto anapozaliwa  hadi pale mtoto atakapofikisha miaka miwili.

Katika mkoa huu wa Dodoma imeonekana kuwa Tatizo hili la kuzaliwa kwa watoto wenye mtindio wa akili lipo kwa asilimia 37 jambo ambalo linapelekea kuongezeka kwa watoto wa mtaani kutokana na watoto hao kutokuelewa  masomo wakiwa darasani na kusababisha kukimbia shule.

Pia amefafanua kuwa Tatizo la  kuzaliwa kwa watoto wenye kasoro kimaumbile linaanzia pale mimba inapotungwa bila mama kujiandaa na hivyo kuwataka kinamama kutumia vidonge vya FOLIC ACID ambavyo vinamkinga mtoto kupatwa na maambukizi ya mangonjwa mbalimbali .

Aidha Bi. Mwita ametoa ushauri kwa wazazi kunyonyesha watoto wao kwa kipindi cha miaka miwili na nusu kutokana na lishe inayopatikana katika maziwa ya mama ambayo  inamjengea afya mtoto huyo tofauti na vyakula vingine ambavyo vinaweza vikamsababishia kuugua utapiamlo. 

Na ANIPHA RAMADHAN                                CHANZO:DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...