Skip to main content

ZAIDI YA WATU ELFU NNE WAKOSA MAKAZI KUFUATIA MAFURIKO WILAYANI CHEMBA DODOMA

                                 Image result for mafuriko katika wilaya ya chemba


Mkuu wa wilaya ya chemba mkaoni Dodoma bwana Simon Odunga amezilalamikia kamati za mazingira katika wilaya yake kwa kuto kuwajibika ipasavyo hali iliyosababisha zaidi ya watu elfu nne kukosa makazi mpaka sasa kutokana na mafuriko.

Bwana Odunga ameyasema hayo wakati akizungumza na DODOMA FM HABARI  juu ya tatizo la mafuriko lililopelekea kuezuka kwa nyumba kadhaa huku wananchi wakikosa makazi.

Mkuu huyo wa wilaya ameonekana akisikitishwa na utendaji kazi wa kamati za mazingira kuanzia ngazi ya wilaya mpaka ngazi ya kijiji.
Amesema amekuwa akihamasisha kamati hizo pamoja na wananchi kuto kuharibu mazingira ikiwemo kufanya shughuli za kilimo milimani lakini tatizo ni kamati hizo kushindwa kufanya ufuatiliaji.

Hata hivyo amesema kamati hizo zimekuwa zikifanya kazi kinyume cha taratibu kwani wakati mwingine anapobainika mtu anahusika na uharibifu wa mazingira na kupelekwa kwenye vyombo vya sheria kamati hizo zimekuwa zikiwatetea jambo ambalo halitakiwi.

Bwana Odunga amesema kuna mpangango mpya ambao wameanzisha kwa sasa wa kuhakikisha wanarejesha uoto wa asili katika eneo la mrijo ambalo limeathirika na mafuriko na kuwataka waathirika wa mafuriko hayo kuhama haraka iwezekanavyo.

Mapema mwezi wa February yaliripotiwa mafuriko katika wilaya ya Chemba eneo la mrijo mkoani Dodoma yaliyosababishwa na mvua hali iliyopelekea kuanguka kwa kaya 570 mpaka sasa.

Na Benard Filbert                                                          Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...