Skip to main content

ZAIDI YA WANAFUNZI MIA NANE WALIOFAULU KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA MJINI DODOMA HAWAJARIPOTI SHULENI MPAKA SASA


                                 Image result for DODOMA YETU


Wito umetolewa kwa wazazi na walezi katika manispaa ya Dodoma kuwapeleka shule wanafunzi waliochaguliwa kuanza kidato cha kwanza kabla ya tarehe ya mwisho iliyopangwa.

Wito huo umetolewa na Afisa elimu sekondari wa manispaa ya Dodoma  ABDALLAH MEMBE wakati akizungumza na Dodoma FM kupitia kipindi cha Taswira ya Habari  juu ya tathmini ya wanafunzi ambao ambao tayari wameripoti shuleni mpaka sasa.

Bwana Membe amesema kuwa baadhi ya wazazi na walezi  hushindwa kuwapeleka wanafunzi kidato cha kwanza kwa sababu zisizo za msingi na hivyo kumnyima mtoto haki yake ya msingi.

Bwana MEMBE amesema kuwa kutokana na baadhi ya wazazi kuwa na  muamko mdogo wa elimu wamekuwa wakiwanyima watoto wao fursa ya kuendelea na masomo pindi wanapohitimu  elimu ya msingi na badala yake huwasafirisha katika mikoa tofauti kwenda kufanya kazi za ndani huku wengine wakibaki nyumbani na kufanya shughuli za kilimo na kuchunga mifugo.

Aidha afisa huyo amebainisha kuwa kutokana na jumla ya wanafunzi 6559 waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule 37 za serikali manispaa ya Dodoma kwa mwaka huu ni wanafunzi 5710 ambao tayari wameanza shule huku wakisalia wanafunzi 849 ambao hawajaripoti kwenye shule walizopangiwa mpaka sasa.

Hata hivyo amewataka wazazi na walezi kutoa taarifa pale mwanafunzi anapoanzishwa kidato cha kwanza katika shule binafsi kwani kutofanya hivyo ni kosa kisheria na adhabu kali huchukuliwa dhidi ya anayekiuka masharti.

Na RWEIKIZA KATEBALIRWE                                      DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...