Skip to main content

YANGA WAWANIA BILIONI 1.1

 

                           

YANGA SC leo inaingia kwenye mtihani wa kwanza wa kuwania Dola za Kimarekani 550,000 zaidi ya Sh. Bilioni 1.1 iwapo wataingia hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

  Wana Dar es Salaam hao leo wanawakaribisha Township Rollers ya Botswana katika mechi ya kwanza ya Raundi ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika Uwanja wa Taifa, Jijini kuanzia Saa 10:00 jioni. 

  Mchezo huo unatarajiwa kuwa mgumu kutokana na ukweli kwamba, Yanga watakutana na timu nzuri, Rollers iliyoiondoa mashindano El Merreikh ya Sudan kwa jumla ya mabao 4-2, ikishinda 3-0 Gaborone na kwenda kufungwa 2-1 Khartoum.

 

Yanga SC yenyewe ilipita kwa mbinde hatua hii, ikishinda 1-0 Dar es Salaam na kwenda kupata sare ya 1-1 Mahe, Shelisheli mbele ya Saint Louis Suns United. 
Habari njema kwa Yanga leo tu ni kwamba, kiungo mtaalamu, Mzimbabwe Thabani Scara Kamusoko aliyekuwa majeruhi kwa muda mrefu sasa yuko fiti na baada ya kufanya mazoezi na wenzake kwa juma zima, anaweza kuwa sehemu ya mchezo wa leo.

 
Pamoja naye, viungo wengine, mzawa Juma Mahadhi na Mzambia, Obrey Chirwa ambao wote wamekuwa wakitumika kama washambuliaji kwa sasa kutokana mapungufu ya wachezaji katika idara hiyo nao wote wako fiti baada ya kukosekana kwenye mechi tatu zilizopita.

 
Mahadhi alifunga bao pekee la ushindi dhidi ya St Louis kwenye mechi ya kwanza Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Februari 10 baada ya hapo akakosekana katika mchezo wa marudiano siku 10 baadaye kutokana na homa.
Mahadhi aliye katika msimu wake wa pili Yanga SC tangu asajiliwe kutoka Coastal Union ya Tanga, alifunga bao hilo dakika ya 66 kwa shuti akimalizia kona iliyopigwa na winga Geoffrey Mwashiuya iliyozua kizazaa langoni mwa Saint Louis.

 
Mahadhi alifunga bao hilo dakika moja baada ya kuingia kuchukua nafasi ya Ibrahim Ajib Migomba kama ilivyokuwa kwa mpishi wa bao lake, Mwashiuya ambaye naye alimbadili Emmanuel Martin

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...