Skip to main content

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAFANIKIWA KUPUNGUZA UJANGILI NA KUONGEZA IDADI YA WATALII

                           Image result for WAZIRI KIGWANGALA
                 
Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt Hamis Kigwangala amesema wizara itaendelea kupambana na ujangili ,biashara haramu ya nyara pamoja na usafirishaji wa magogo.

Ameyasema hayo mapema leo mjini  Dodoma wakati akifungua mkutano wa 25 wa baraza la wafanyakazi wa  wizara ya Maliasili na Utalii ambapo amesema kuwa  serikali haitosita kuchukua hatua kali kwa watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo.

Waziri Kigwangala amesema hivi karibun kumekuwepo na taarifa za ujangili ,usafirishaji haramu wa magogo na wanyama pori vinavyofanywa na wananchi wasio na uzalendo kwa kushirikiana na baadhi ya watumishi wa wizara jambo ambalo limekuwa likiipotezea serikali mapato hivyo kusaababisha kurudisha nyuma jitihada za kuimarisha uchumi wa Taifa.

Akizungumzia mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa wizara kwa kipindi tofauti Dkt Kigwangala amesema kuwa matukio ya ujangili,biashara haramu ya rasilimali za misitu na wanayama pori yamepungua kwa kiasi kikubwa ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa idadi ya watalii kutoka milioni 1,284,279 mwaka 2016 hadi kufikia milioni 1,327,143 kwa mwaka 2017.

Awali akisoma taarifa ya wizara kwa waziri Kigwangala katibu mkuu wizara ya maliaslili na utalii meja Jenerali Gaudience Milanzi amesema kuwa tayari wizara imekwisha kuanza mchakato  wa kuazisha jeshi maalumu litakalosimamia rasilimali zote katika maeneo yote ya hifandhi nchini na amewasihi watumishi wote kutekeleza majukumu yao ipasavyo ili kufikia malengo.

NA ALFRED BULAHYA                                                DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...