Skip to main content

WAZIRI MBARAWA ASEMA SERIKALI HAITAMVUMILIA MTUMISHI ATAKAYEKWAMISHA BAJETI

                                   Image result for WAZIRI MBARAWA


Waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano prof Makame Mbarawa amesema serikali haitasita kumchukulia hatua mtumishi yeyote atakayeonekana kuwa chanzo cha kukwamisha malengo ya bajeti wakati wa kufanya mapitio ya bajeti ya nusu mwaka hapo baadae.

kauli hiyo imetolewa leo na Eng. Joseph Nyamhanga alipokuwa akitoa hotuba kwa niaba ya Waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano prof Makame Mbarawa wakati wa kufungua mkutano wa baraza la wafanyakazi wa sekta ya uchukuzi mjini Dodoma.

Amesema kuwa serikali itakapokuwa ikifanya mapitio ya bajeti ya nusu mwaka hapo baadae na kugundua uwepo ukiukwaji wa taratibu zilizowekwa haitosita kumwajibisha mtumishi yeyote atakayeonekana kutotimiza malengo ya bajeti hiyo hivyo ni vyema watumishi wakazingatia maelekezo ili kila mmoja atekeleze majukumu yake ipasavyo.

Hata hivyo ameitaka menejimenti ya wizara na chama cha wafanyakazi TUGHE kuhakikisha kuwa zinafanya kazi kwa mshikamano thabiti katika kufikia maamuzi mbalimbali ya kisera na kitaaluma ambayo yatafanikisha shughuli za sekta ya uchukuzi na tabiri za hali ya hewa kufikia malengo yao.

Awali akisoma taarifa ya baraza la wafanyakazi wa sekta ya uchukuzi mwenyekiti wa baraza la wafanyakazi la wizara ya uchukuzi dkt Leonard Chamriho amesema kuwa sekta ya uchukuzi kwa mwaka mpya wa fedha unaokuja 2017/18 imejiwekea malengo ya kuboresha miundombinu ya hali ya hewa, ununuzi wa ndege mpya 4 kwa ajili ya kuboresha huduma za ATCL pamoja na kutekeleza awamu ya pili na ya tatu ya serikali kuhamia Dodoma.

Na Alfred Bulahya                                                         DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...