Skip to main content

WATUMISHI NCHINI WASHAURIWA KUJIUNGA NA VYAMA VYA MIKOPO

                                             Image result for SACOSS


Katibu  mkuu wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga Taifa Dk.Florence Tuluka amewataka watumishi nchini kujiunga na vyama vya akiba na mikopo (SACCOS) ili kupata nafuu ya maisha  watakapostaafu.

Katika ufunguzi wa semina ya wakuu wa vyuo,shule na makamanda wa vikosi iliyofanyika  mkoani Dodoma Dr Florence amesema  kila mtumishi ana wajibu wa kujiwekea akiba pia kukopa katika saccos kutokana na riba nafuu zinazotolewa ambazo zipo tofauti na maeneo mengine wanayokopesha.

Aidha amesema Pamoja na elimu ya ushirika na ujasiliamali inayotolewa lakini kila mmoja ana wajibu wa kujiunga na Ngome Saccos ili kujiwekea akiba na kupata mikopo kwa kuwa mtumishi yeyote ni mstaafu mtarajiwa.

Tuluka ameongeza kuwa semina wanayoifanya itawawezesha kufahamu utendaji  kazi wa SACCOS pia itawashawishi wakuu ambao hawajajiunga na chama hicho cha kuweka na kukopa waweze kujiunga.

Hata hivyo amesema  elimu ya ushirika ambayo itatolewa ina umuhimu wa kipekee katika kuujenga ushirika imara na itawaongoza katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

NGOME  SACCOS  ilipata usajili mwaka 1967 na kuanza kutumika mwaka 2007 ikiwa na lengo la  kutoa mikopo ya dharura, mikopo ya maendeleo na mikopo ya wastaafu.

Mariam Matundu                                                Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...