Skip to main content

WATU WAWILI MJINI DODOMA WANASHIKILIWA NA JESHI LA POLISI KWA KUHAMASISHA MAANDAMANO

                                   Image result for WAKAMATWA KWA KUHAMASISHA MAANDAMANO DODOMA 


Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma linawashikilia watu wawili kwa kosa la matumzi mabaya ya mitandao ya kijamii kwa kuhamasisha maandamano haramu yaliyopangwa kufanyika Nchini tarehe 26 Aprili mwaka huu.

Kamanda wa jeshi la polisi Mkoa wa Dodoma Gilles Muroto ameyasema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Dodoma na kueleza kuwa vijana hao wamebainika kusambaza taarifa za kuhamasisha maandamano ya nchi nzima yenye viashiria vya uchochezi dhidi ya Serikali na kutishia usalama wa nchi.

Amewataja waliokamatwa kuwa ni pamoja na Amandus Manchali mwenye umri wa mika 31ambae ni dereva wa shirika la bima ya afya NHIF pamoja na kijana Yuda Mbata mwenye umri wa miaka 29 mkazi wa Kijiji cha mpamatwa Wilaya ya Bahi Mkoa wa Dodoma.

Kamanda Muroto amesema maandamano hayo yanayohamasishwa msingi wake ni kusababisha uhalifu, kuhatarisha amani ya nchi, kuhatarisha usalama wa raia na mali zao na kutoa wito kwa wananchi kujiepusha na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii badala yake mitandao hiyo itumike kuchochea na kuharakisha maendeleo.

Baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Dodoma wakizungumza na kituo hiki wamesema bado elimu juu ya matumizi sahihi ya mitandao ya kijamii inapaswa kuendelea kutolewa ili wananchi waweze kunufaika na uwepo wa mitandao hiyo badala ya kuitumia katika matumizi yasiyokuwa sahihi.

Katika hatua nyingine Kamanda Muroto amesema kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha Mkoani Dodoma zimesababisha vifo vya watu watatu wote wa familia moja katika Kijiji cha Gwandi Wilaya ya Chemba na kutoa wito kwa wananchi kuchukua tahadhari mapema ikiwemo kuto kuvuka mito iliyo jaa maji.

Na Pius Jayunga                                                    DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...