Skip to main content

WATU 200 HADI 225 WANAAMBUKIZWA UKIMWI KWA SIKU NA ASILIMIA 40 NI VIJANA


                                                 Image result for UKIMWI


Jumla ya watu 200 hadi 225 wanapata maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi kwa siku ambapo asilimia 40 kati yao ni vijana wenye umri kati ya miaka 15-24 na kati ya hao vijana jumla ya asilimia 80 ni vijana wa kike.

Takwimu hizo pia zimo katika ripoti ya tathimini ya mazingira ya kisheria katika mwitikio wa ukimwi iliyozinduliwa desemba mosi mwaka jana katika siku ya ukimwi duniani

Akielezea matokeo ya utafiti huo  mjini dodoma mkurugenzi mtendaji wa tume ya kudhibiti ukimwi nchini (TACAIDS) Dk.Leonard Maboko wakati wa kikao cha siku mbili kwa ajili ya usambazaji wa ripoti hiyo ameeleza kuwa jumla ya watu elfu 81 wanapata maambukizi mapya kwa mwaka ambayo ni sawa na wastani wa watu 225 kwa siku.

Dr Maboko amesema katika tafiti zilizofanywa kwa mwaka 2016/17 zinaonyesha asilimia 91 ya waathirika wanaojua hali zao wamekwisha anza dawa na asilimia 88 kati yao wamekwisha fubaza virusi vya ukimwi  jambo ambalo lipo katika hatua nzuri  huku akiongeza kuwa wanaume ndio  wanaoongoza kwa kutopima VVU.

kwa upande wake mkurugenzi wa ufatiliaji na tathimini (TACAIDS ) Jerome Kamwela amesema asilimia 80 ya maambulkizi ya ukimwi tanzania yanatokana na mahusiano ya kingono na waliosalia hupata maambukizi kwa njia nyinginezo ambapo pia ameelezea idadi ya watanzania wanaoishi na virusi vya ukimwi hadi hivi sasa.

Na Mariam Matundu                                             Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...