Skip to main content

WANAWAKE WAHIMIZWA KUSHIRIKI KIKAMILIFU KUCHOCHEA UCHUMI WA VIWANDA


                                           Image result for wanawake Dodoma


Wanawake mjini Dodoma wametakiwa kujituma kushiriki katika shughuli mbalimbali za maendeleo ili kuendana na kasi ya serikali ya awamu ya tano yenye lengo la kuwa na serikali yenye uchumi  wa viwanda.

Kauli hiyo imetolewa leo ma mbunge wa viti maalum mjini Dodoma Mh Fatuma Toufiq wakati akitoa hotuba katika kilele cha maadhimisho ya wanawake duniani yaliyofanyika Kimkoa katika viwanja vya kata ya Msalato Mjini Dodoma.

Mh Toufiq amesema kuwa  taifa linakabiliwa na chanagamoto nyingi hivyo ni vyema wanawake wote wakaacha tabia ya kuwa wasindikizaji bali wawe watendaji hali ambayo itawasaidia kufikia malengo kwa pamoja  katika uchumi wa viwanda.

KATIKA hatua nyingine Toufiq amezindua mpango kazi wa miaka 3 utakaosimamia jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi ili kukabiliana na changamoto zinazowakabili hali itakayowasaidia kuendeleza na kukuza ujasiria mali pamoja na biashara zao.

Awali akisoma risala mratibu wa dawati la uwezeshaji wananchi kiuchumi kutoka manispaa ya Dodoma Bi Hidaya Mizega amesema kuwa wanawake wanapaswa kuzitambua fursa zilizopo na kuzitumia.

Maadhimisho ya wanawake duniani huadhimisha kila mwaka ifikapo machi 8 na kwa mwaka huu mkoani Dodoma yameadhimishwa katika kata ya Msalato huku yakiwa yamebebwa na kauli mbiu isemayo kuelekea uchumi wa viwanda tuimarishe usawa wa kijinsia kwa wanawake vijijini.

Na Alfred Bulahya                                          Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...