Skip to main content

WANAWAKE LAKI 6 HUPOTEZA MAISHA KUTOKANA NA MATATIZO YA FIGO


                                               Image result for magonjwa ya figo


Magonjwa ya figo yanakadiriwa kuwaathiri takribani wanawake milioni 195 duniani kote na yanashika nafasi ya 8 .

Chanzo cha vifo vya wanawake duniai na inakadiriwa kuwa wanawake laki 6  hupoteza maisha kutokana na matatizo ya figo duniani kote kila mwaka.

Naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Dk. Faustine Ndugulile ameyasema hayo wakati akitoa tamko la siku ya figo Duniani na kusema tafiti zilizofanywa na shirika la afya Duniani (WHO) zinaonyesha wanawake wako katika hatari zaidi ya kupata matatizo ya figo ikilinganishwa na wanaume kwa wastani wa 14% ya wanawake wanaathiriwa na matatizo ya figo ikilinganishwa na asilimia 12 kwa wanaume.

Amesema utafiti uliofanywa na hospitali ya kanda ya Bugando umeonesha kuwa 83% ya wagonjwa wa kisukari wana matatizo sugu ya figo na kati yao 25% wanahitaji huduma za usafishaji damu huku mgonjwa mmoja akigharimu fedha kiasi cha sh. Mil. 37  kwa wastani wa safari 126 kwa mwaka.

Pamoja na hayo Dr. Faustine ametoa wito kwa wananchi kubadili jinsi ya kuandaa chakula majumbani kwa kupunguza kiasi cha chumvi katika chakula na kiasi cha mafuta ili kupunguza ugonjwa wa shinikizo la damu kisukari na unene uliopitiliza na kuhamasisha familia kujenga mazoea ya kufanya mazoezi ya viungo mara kwa mara.

Kwa upande wake Rais wa chama cha madaktari bingwa wa figo Nchini Dr. Onesmo Kisanga amesema lengo la chama cha madaktari wa figo hapa Nchini ni kuelimisha wananchi juu ya umuhimu wa afya ya figo na ikiwemo swala la upimaji wa figo na tatizo la ugonjwa huo likitajwa kusababishwa na magonjwa nyemelezi kama ugonjwa wa moyo na kisukari hususani kwa upande wa  kina mama.

Maadhimisho ya siku ya figo huadhimishwa kila mwaka tarehe 8 mwezi march na mwaka 2018 maadhimisho hayo yamebebwa na kauli mbiu isemayo figo na afya ya wanawake: washirikishwe, wathaminiwe na wawezeshwe.

Na Pius Jayunga                                                       Dodoma FM

Comments

  1. Hakika tunapaswa kuchukua tahadhari kwa kupima afya zetu mara kwa mara.

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madiwani ambapo baadhi yao wametoa maoni tofauti tofauti juu ya ufafanuzi huo. Kufuatia hayo katibu  tawala msaidizi mkoa anayesh

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifugua kwa upasuaji na

SERIKALI IMEANZA KUANDAA KITINI CHA MASUALA YA JINSIA

                                             Serikali imeanza mchakato wa kuandaa kitini cha masuala ya jinsia kuendeleza kasi ya utekelezaji wa mpango wa kitaifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Akizungumza katika kikao cha wataalam na wadau wa maendeleo ya Jinsia Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Jinsia Bi. Mboni Mgaza amesema Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto umekithiri sana nchini   hivyo Serikali kuamua kutafuta njia tofauti za kupambana na tatizo hilo. Amesema   lengo la kuandaa kitini cha kufundishia masuala ya Jinsia “ni kwa ajili ya utekelezaji wa Mpango Kazi wa Kitaifa wa kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto ambao utatoa uelewa kwa wadau wa maswala ya jinsia na maafisa Maendeleo ya Jamii kuanzia ngazi ya Mkoa, Halmashauri na kata ili kutoa elimu ya masuala ya Jinsia katika jamii. Bi. Mboni amefafanua kuwa kwa mujibu wa takwimu ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 idadi ya wanawake nchini ilikuwa ni Milioni Is