Skip to main content

WANAUME WASHAURIWA KUTOA TAARIFA WANAPOFANYIWA UKATILI.



                             Image result for UKATILI KWA WANAUME

Wanaume mkoani Dodoma wameshauriwa kuwa na desturi ya kutoa taarifa katika vyombo vinavyosimamia masuala ya ukatili, pindi wanapofanyiwa ukatili ili kuendelea kutokomeza ukatili katika jamii.

Kauli hiyo imetolewa leo na mwanasheria kutoka katika taasisi ya sheria ya DARWINS ATORNEY AND CONSULTANTS ya mjini Dodoma bw Chrispin Nicholaus Rwila wakati akizungumza na kituo hiki ofisin kwake.

Amesema kuwa wanaume wengi wamekuwa hawana desturi ya kutoa taarifa kwa vyombo husika pindi wanapofanyiwa ukatili, kutokana na kuogopa fedheha jambo ambalo linaweza kusababisha madhara makubwa kama msongo wa mawazo na hata kifo.

Akizungumzia sheria inayosimamia suala la ubakaji amesema kuwa sheria hiyo haijaweka wazi namna ya kuwasaidia wanaume pindi wanapokumbwa na tatizo hilo, ambapo ameiomba serikali kulitazama jambo hilo kwa jicho la tatu ili kuweka usawa kwa wananchi wote.

Nao baadhi ya wakazi wa mji wa Dodoma wameiambia Dodoma Fm kuwa suala la wanaume kutotoa taarifa pindi wanapofanyiwa ukatili, linatokana na baadhi yao kuona aibu kutokana na kujijengea mazingira ya kuamini kuwa mwanaume ndiyo kichwa cha familia, hivyo akionekana anatoa taarifa za kufanyiwa ukatili anaweza kufedheheka.

Na Alfred Bulahya                                                                   DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...