Skip to main content

WANANCHI WAHIMIZWA KUZIJUA SHERIA ZA UMILKI ARDHI ILI WASIDHULUMIWE



                      Image result for SHERIA ZA UMILIKI ARDHI


Kuto kuwa na uelewa juu ya masuala ya umiliki wa ardhi kwa baadhi ya wakazi nchini umetajwa kuwa ni sababu mojawapo inayosababisha  migogoro ya ardhi katik.

Hayo yameelezwa na mwanasheria na wakili wa kujitegemea Bwana Saidy Kamsumbile alipokuwa akizungumza na Dodoma FM ambapo amebainisha kuwa  tatizo la migogoro ya ardhi ni la muda mrefu isipokuwa kuna baadhi ya wananchi hawana uelewa juu ya sheria za umiliki ardhi.

Bwana Kamsumbile amesema sheria hizo ni muhimu kwa wanachi wakazitambua kwa sababu wakazi wengi hukumbwa na sintofahamu pale wanapo kumbwa na migogogoro ya ardhi na hatimaye kushindwa kujua kama anahaki ya kushinda kesi mahakamani au kushindwa.

Pamoja na hayo amesema kuna baadhi ya wananchi wanajitahidi kutembelea katika ofisi mbalimbali za wanasheria kwa lengo la kutaka kujua sheria juu ya umiliki wa ardhi lakini wanalazimika kutoa pesa ndipo wapatiwe elimu hiyo kitu ambacho sio haki.

Sanjari na hayo amewataka wananchi kuwa makini pindi wanaponunua ardhi ikiwa ni pamoja na kuhakikisha eneo ambalo unanunua limepimwa na mamlaka husika ili kuepusha migogoro.

Miongoni mwa wakazi mkoani hapa akiwepo bwana Issa Rajabu amesema kuna umuhimu kwa kila mwananchi kujua sheria angalau hata kidogo ili kusaidia kujitetea pindi upatapwo na matatizo.

Kila mwaka wizara ya katiba na sheria wadau wa maendeleo na mashirika yasiyo ya kiserikali yanayojihusisha na utoaji wa huduma ya msaada wa kisheria nchini huadhimisha maadhimisho ya wiki ya msaada wa kisheria lengo kubwa ni kutoa elimu kwa umma pamoja na watu mbalimbali waliopo polisi na gerezani.

Na Benard   Filbert                                                       Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...