Skip to main content

TCRA YAWASHAURI WANAFUNZI WASITUMIE MITANDAO WAWAPO SHULENI

                          Image result for MAMLAKA YA MAWASILIANO


Mamlaka ya mawasiliano Tanzania  TCRA imewataka wanafunzi walioko chini ya umri wa miaka 18 kutojihusisha na suala la matumizi ya mitandao wakiwa shuleni na badala yake kutumia muda huo kujifunza zaidi ili kuwa watumiaji wazuri wa baadae.

Hayo yamesema na naibu mkurugenzi wa huduma na bidhaa za mawasiliano kutoka mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA Bw. Thadayo Ringo wakati akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari ya wasichana ya Msalato mjini Dodoma katika maadhimisho ya siku ya haki na wajibu kwa watumiaji wa mitandao ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo march 15.

Awali akitoa elimu kwa watumiaji wa huduma za mawasiliano afisa masafa kutoka ofisi ya mamlaka ya mawasiliano mjini Dodoma Boniphace Ngeela amewaasa wananchi kuacha tabia ya  kusambaza taarifa mbalimbali zinazoweza kuleta mkanganyiko katika jamii kwani  ni wajibu wa kila mtumiaji kuhakikisha anatumia vizuri simu yake ili kuondoa adha kwa watumiaji wengine.

Mkuu wa shule ya sekondari Msalato Mwalimu Line Chanafi amepongeza hatua zinazofanywa  na mamlaka ya mawasiliano za kuhakikisha watumiaji wanatumia huduma za mawasiliano kwa usahihi huku akitumia nafasi hiyo kuwataka wanafunzi wote kusoma kwa bidii ili kufika katika kilele cha mafanikio waliyoyakusudia.

NA ALFRED BULAHYA                                                 DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...