Skip to main content

WANAFUNZI WANAOHITIMU DARASA LA SABA MWAKA HUU KUFANYA MTIHANI WA KUJIELEZA


                                   Image result for UTUNGAJI MTIHANI DARASA LA SABA WABADILISHWA


Imeelezwa kuwa kubadilishwa kwa utungaji wa Mtihani wa kuhitimu Darasa la saba kwa mwaka  2018 kutoka maswali ya kuchangua pekee mpaka mwaswali ya kuchagua na kujieleza kutawasaidia wanafunzi kujijengea uwezo wa ufahamu.

Akiongea na Dodoma Fm Afisa Elimu Msingi anaesimamia Taaluma katika Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma Mw. Mlavi Ramadhan amesema lengo la Baraza la Mitihani ni kutaka kupima uelewa wa wanafunzi katika masomo wanayofundishwa darasani  na kwamba mfumo uliopo utakuwa ni kipimo tosha kwa mwanafunzi.

Mw. Ramadhan amesema  mara baada ya kupokea  maelekezo hayo kutoka baraza waliwasiliana na walimu wakuu na kuagiza kwa kila mazoezi ya mitihani yatakayotolewa kwa wanafunzi yatungwe kwa kutumia  mfumo mpya uliotangazwa na baraza la Mitihani.

Sambamba na hayo amewataka walimu wa Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma kufanya kazi kwa bidii pamoja na kubadilisha mifumo yao ya ufundishaji na kufundisha kulingana na muundo wa mitihani ya sasa itakavyotungwa.

March 20 mwaka huu baraza la Mitihani la Taifa(NECTA) kupitia katibu mtendaji wa Baraza hilo Dk Charles Msonde  alisema Wanafunzi wa darasa la saba ambao watafanya mtihani mwaka huu watakutana na mabadiliko ya mfumo wa utungaji  wa mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi .

Na Phina Nimrod                                             Dodoma fm

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...