Skip to main content

WALIMU WATAKIWA KUUNGA MKONO JITIHADA ZINAZOFANYWA NA SERIKALI KUBORESHA SEKTA YA ELIMU

                          Image result for shirika la young scientist


Wito umetolewa kwa walimu nchini kuhakikisha wanajikita katika kutoa mafunzo yenye uhalisia kwa wanafunzi yenye uwezo wa kukabiliana na changamoto zao za  kimaisha .

Wito huo umetolewa Jana na afisa elimu kutoka wizara ya elimu sayansi na teknolojia bw Fundikira Ekerele wakati akizungumza katika warsha fupi iliyoandaliwa na shirika la YOUNG SCIENTIST TANZANIA (YST) linalojishughulisha na utoaji wa elimu ya sayansi kwa walimu iliyowakutanisha walimu mbalimbali  kutoka mikoa ya Dodoma ,Singida na Morogoro.

Amesema kuwa sera mpya ya elimu na mafunzo imeweka msisitizo kwa walimu kujikita katika ufundishaji utakaomjengea uwezo mwanafunzi wa kukabiliana na changamoto za kimaisha anapomaliza masomo yake ili kuepusha wimbi la vijana wasiokuwa na kazi mitaani.

Kwa upande wake msimamizi wa elimu kutoka wizara ya elimu ofisi ya rais tawala za mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI BW Ndabazi Stephano amesema kuwa ili kufikia uchumi wa kati ifikapo 2020 walimu na wadau wote wanatakiwa kuunga mkono juhudi zinazofanyika katika kuboresha sekta ya elimu nchini.

Meneja wa taasisi ya Karimjee (JIANJEE FOUNDAION) bi Devota Rubama ambao ndio wafadhili wakuu wa Shirika la YOUNG SCIENTIST TANZANIA (YST amewaomba wadau mbalimbali kujitokeza kuunga mkono juhudi zinazofanywa na taasisi hiyo huku akitaja sababu zilizowasukuma kutoa ufadhili kwa shirika hilo.

Taasisi YOUNG SCIENTIST TANZANIA (YST) ilianzishwa mwaka 2011 kwa lengo la kuwasaidia wanafunzi wa shule za sekondari kupata elimu ya sayansi na teknolojia inayotakiwa ili kupata wanasayansi mahili watakaoweza kuja na masuluhisho mbalimbali ya matatizo yanayolikabili taifa la tanzania.

NA ALFRED BULAHYA                                        DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...