Skip to main content

WALIMU AMBAO HAWATAFUATA TARATIBU ZA RUHUSA WANAWEZA KUFUKUZWA KAZI


                                        Image result for walimu



Waajiri wa walimu katika shule za Msingi na Sekondari za umma kote Nchini wakiwemo wakurugenzi wa halmashauri za Wilaya, Manispaa na  Miji, wametakiwa kufuata sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma katika utoaji wa vibali vya ruhusa kwa walimu.

Katibu wa tume ya utumishi wa walimu Nchini Bi. Winifrida Rutaindurwa ametoa maagizo hayo leo wakati akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake Mjini Dodoma ambapo amesema kumekuwa na mazoea ya waajiri kutoa ruhusa ya mdomo au  makubaliano kwa njia ya simu jambo ambalo ni kinyume na utaratibu.

Aidha amekemea tabia ya baadhi ya walimu Nchini kuondoka katika vituo vyao vya kazi kwenda masomoni bila kibali cha mwajiri na kibali hicho kinatakiwa kuwa katika maandishi huku akiwataka walimu kuzingatia muda wa kurudi katika vituo vyao vya kazi mara baada ya kuhitimu masomo yao.

Ameongeza kuwa maafisa elimu Nchini wanapaswa kutambua majukumu yao kuwa ni pamoja na kuwashauri waajiri wa walimu katika halmashauri na kwamba ni wajibu wao kuhakikisha walimu wa shule za msingi na sekondari za umma wanahudumiwa kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za Nchi.

Kwa upande wake afisa sheria wa tume ya utumishi wa walimu Nchini Wakili Deogratius Osmasi Haule amesema ni kosa kisheria kwa mwalimu kuondoka katika kituo chake cha kazi bila kibali cha mwajiri ikiwa ni pamoja na ruhusa hizo kuwa katika mfumo wa maandishi huku mwajiri akitakiwa kutoa ruhusa mapema ili kuepusha madhara ambayo huwenda yakatokea kwa mwalimu ikiwemo kushushwa kazi, kushushwa mshahara pamoja na kufukuzwa kazi.

Na Pius Jayunga                                                         Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...