Skip to main content

WAGANGA WA TIBA ASILI WATAKAOHUSIKA NA UPIGAJI RAMLI KUKIONA

                                  Image result for UPIGAJI RAMLI


Mwenyekiti wa shirikisho la vyama vya tiba asili Tanzania amesema shirikisho hilo halitasita kumchukulia hatua za kisheria mganga yeyote wa tiba asili atakaejihusisha na kupiga ramli chonganishi.

Bw. Abdalaman Mussa Lutenga ameyasema hayo kufuatia Serikali kupitisha matumizi ya dawa za tiba asili zilizo thibitishwa na mkemia mkuu wa Serikali kuwa zinaweza kutibu tatizo la nguvu za kiume na hivyo huwenda baadhi ya waganga wakatumia mwanya huo kukiuka sheria za tiba asili kitendo ambacho hakitavumiliwa.

Amesema sheria ya tiba asili inapinga matumizi ya tiba zitokanazo na ramli chonganishi ambazo huchangia kwa kiasi kikubwa kuchonganisha watu na kuvunja sheria namba 23 kifungu cha 30 kinachozuia mganga kutoa huduma ya tiba asili kwa njia ya ramli.

Bw.Lutenga amesema shirikisho la vyama vya tiba asili Tanzania litaendelea kuelimisha waganga hao ili kuitambua sheria na kwamba elimu hiyo imekuwa ikifikishwa kwa waganga katika Mikoa yote Tanzania ili kuwaepusha kujihusisha katika ramli chonganishi.

Ikumbukwe kuwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na Watoto, Dk Faustine Ndugulile amekwisha kumuagiza Katibu Mkuu Wizara ya Afya akishirikiana na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), kufanya utafiti wa afya ya uzazi kwa wanaume ili kubaini sababu za tatizo hilo na kujua ongezeko la upungufu wa nguvu za kiume ni kubwa kiasi gani nchini.

NA PIUS JAYUNGA                                              DODOMA FM


Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...