Skip to main content

WAGANGA WA KIENYEJI KUSAIDIANA NA SERIKALI KUWABAINI WAGONJWA WA TB


                                        Image result for ugonjwa wa kifua kikuu


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto UMMY MWALIM amewataka viongozi wa serikali za vijiji vyote Tanzania kuwaandikisha waganga wa kienyeji waliopo katika maeneo yao kushirikiana kuwapata watu wenye ungojwa wa TB waliopo maeneo mbalimbali ili kuwapatia matibabu bora zaidi.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini DODOMA Kuelekea maadhimisho ya siku ya kifua kikuu duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo march 24, Waziri Ummy amesema Kutokana na ugonjwa wa kifua kikuu kuwa tatizo kubwa hapa nchini wamekusudia kushirikiana na waganga wa kienyeji  ili wasaidie katika kuwabaini wagonjwa wa kifua na kupewa matibabu stahiki.

Waziri UMMY amesema wanahitaji kuongeza nguvu ili kukabiliana na  ugonjwa huo kutokana na ukubwa wa tatizo ambapo amethibitisha wagonjwa laki moja na elfu sitini wamebainika huku asilimia aroboini pekee wamefanikiwa kuwapatia matibabu.

Kwa upande wake Meneja mpango wa taifa wa kudhibiti kifua kikuu na ukoma BEATRICE MUTAYOBA ameongeza kuwa wamejipanga kutoa elimu ya kutosha hasa vijijni kutokana na ujenzi duni wa nyumba zisizo na madirisha ya kupitisha hewa za kutosha na kutoa mafunzo kwa waganga wa kienyeji,ikiwa ni pamoja na kuwawezesha kwa  kuwapatia  vitendea kazi kwa ajili ya kutoa rufaa.

Nae Mkurungezi wa kinga DR LEONARD SUBI amebainisha waganga wa tiba asilia wanasajiliwa kisheria na  serikali inaendelea kuhamasisha kushirikiana na waganga wa tiba asilia.

Takwimu za mwaka 2017 zinaonyesha kuwa mikoa 26 asilimia kubwa ya wagonjwa wa kifua kikuu wanatoka  mkoa wa Dar es salaam 20%, Mwanza 6%, mbeya ,arusha,dodoma na morogoro 5% ikifuata na Geita,Tanga,manyara,shinyanga na kilimanjaro 4%  huku  katavi,ugunja na rukwa zikiwa ni asilimia moja.

Waandishi Mindi Joseph na Hadija Halfani                  DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...