Skip to main content

VIJANA KUJIUNGA KATIKA MAKUNDI NA KUFANYA UHALIFU NI CHANGAMOTO KUBWA KATA YA KIZOTA MJINI DODOMA


                                         Image result for Kata Kizota Manispaa ya Dodoma


Makundi ya vijana wanaofanya uhalifu yameibuka katika kata ya kizota Manispaa ya Dodoma na kupelekea hali ya usalama kutokuwa nzuri.

Akizungumza na Dodoma FM Kupitia Taswira ya habari Afisa mtendaji wa kata ya Kizota  Bi LOYCE JOEL amesema  yapo makundi ya vijana kutoka katika mitaa tofauti iliyoko katika kata hiyo kwa kushirikiana na makundi mengine kutoka maeneo jirani na Kizota hutekeleza uhalifu huo hasa nyakati za usiku kwa kuvunja milango na kupora baadhi ya mali za wananchi pindi wanapokuwa wamelala.

Bi LOYCE amesema kutokana na doria inayofanywa na polisi jamii kwa kushirikiana na polisi kata imebainika kuwa makundi hayo yanaundwa na vijana kutoka mitaa ya Mbuyuni na Sokoine huku kundi shiriki kutoka jirani likiwa linatokea Chinangari West.

Amesema makundi hayo ya uhalifu yanashirikisha vijana wadogo kwani  wengi wao wako kati ya umri  wa miaka 16-18 huku akikemea kitendo cha kutolewa kwa dhamana pindi wanapokamatwa na kufikishwa polisi jambo ambalo amesema linapunguza adhabu kwani ilitakiwa wawe wanakaa angalau miezi sita ili kujifunza na kujirudi kimakosa.

Afisa mtendaji huyo ametoa wito kwa wazazi na walezi kuwakanya vijana hao kwani bado wanahitaji malezi kutoka kwao kulingana na umri wao kuwa mdogo kwani kwa kutofanya hivyo sheria itachukua mkondo wake na kuwatia hatiani.

Na RWEIKIZA KATEBALIRWE                                   DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...