Skip to main content

UKOSEFU WA VYUO VYA UFUNDI NI CHANGAMOTO KWA VIJANA WILAYANI KONGWA.


                                            Image result for vyuo vya ufundi



Ukosefu wa vyuo vya ufundi katika Wilaya ya Kongwa Mkoa wa Dodoma ni moja ya sababu zinazokwamisha vijana wengi Wilayani humo kuto kufikia malengo yao.

Baadhi ya vijana katika wilaya ya Kongwa wamebainisha hayo wakati wakizungumza na Dodoma Fm na kueleza kuwa licha ya wao kuwa na ndoto ya kufanikiwa kwa kujishughulisha na shughuli za ufundi bado wanakwama kufanikisha malengo yao kutokana na kuto kuwepo kwa vyuo vya ufundi ambavyo vinaweza kuwaongezea ujuzi zaidi.

Wamesema ni vema Serikali ikatekeleza ahadi zake kwa wananchi Wilayani humo ikiwemo ujenzi wa vyuo vya ufundi ili kutoa fursa kwa vijana kupatiwa elimu na ujuzi wa kufanya kazi kwa maendeleo yao na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa wa Mnyakongo Wilayani Kongwa Bwana Moses Patson amesema ukosefu wa vyuo vya ufundi umechangia vijana wengi kushinda mitaani na baadhi yao wamekuwa wakituhumiwa kujihusisha na vitendo vya uhalifu.

Hata hivyo Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Mhandisi Ngusa  Izengo amesema uongozi wa Wilaya unatambua kuwepo kwa changamoto hiyo na tayari wametoa eneo la ekali 200 kwa jeshi la kujenga Taifa JKT ili kujenga chuo cha ufundi pamoja na ujenzi wa chuo cha maji kupitia Wizara ya maji.

Na PiusJayunga                                                                Dodoma Fm

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...