Skip to main content

UKOSEFU WA CHOO KITUO CHA MABASI KONGWA WAHATARISHA AFYA ZA WANANCHI

                                                  Image result for Wilaya ya kongwa dodoma


Ukosefu wa huduma ya choo katika eneo la kituo cha mabasi cha halmashauri ya Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma kuna hatarisha usalama wa afya za wananchi wanaofika katika eneo hilo.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Mnyakongo shuleni katika Wilaya ya Kongwa Mkoa wa Dodoma Bw. Moses Patson ameiambia Dodoma fm kuwa kufutia kuanzishwa kwa huduma ya stand katika Wilaya ya Kongwa bila huduma ya vyoo ni moja ya sababu zinazoweza kuchangia kutokea kwa magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu.

Amesema Kutokana na wingi wa watu pamoja na ukubwa wa eneo la stendi ni vema uongozi wa Halmshauri ya Wilaya ya Kongwa ukaanza ujenzi wa matundu ya vyoo katika eneo hilo ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wananchi.

Kwa upande wake Mkurugenzi mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Kongwa Mhandisi Ngusa Izengo amesema katika stendi  hiyo kuna choo kilicho jengwa na kubinafisishwa kwa ajili ya usimamizi na kutokana na wingi wa watu uliopo kwa sasa Halmashauri ya Wilaya hiyo inatarajia kuanza ujenzi wa choo kikubwa kitakachotosheleza mahitaji ya wananchi katika eneo hilo.

Mhandisi Igezo amewasihi wananchi kujenga mazoea ya kuchangia kiasi cha fedha kilichoelekezwa na uongozi wa halmashauri ya Wilaya hiyo pamoja na kuepuka kujisaidia hovyo katika maeneo yasiyokuwa rasmi ili kuepusha vimelea vya magonjwa ya kuambukiza ikiwemo kipindupindu.

Na Pius Jayunga                                                         DodomaM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...