Skip to main content

UBOVU WA BARABARA WAPELEKEA WATU KUPOTEZA MAISHA KUTOKANA NA AJALI ZA MARA KWA MARA

     
                                 Image result for UBOVU WA BARABARA MBANDE KONGWA NA MPWAPWA     


Baadhi ya wakazi wa Kata ya Mnyakongo shuleni katika Wilaya ya Kongwa Mkoa wa Dodoma wamelalamikia ubovu wa eneo la makutano ya barabara ya Mbande, Mpwampwa na Kongwa.

Wakizungumza na Dodoma FM wananchi hao akiwemo Jumbe Jarom pamoja na Wilson Batogwa wamesema kutokana na ubovu wa eneo hilo kunachangia kuwepo kwa ajali za mara kwa mara huku ufinyu wa eneo hilo wakati wa kupishana magari pamoja na wingi wa mchanga vikitajwa kuwa ni moja ya sababu za ajali.

Wananchi hao wamebainisha kuwa kuna ajali ambazo zimewahi kutokea katika eneo hilo na kupoteza maisha ya watu huku wakilalamikia ukosefu wa alama za usalama barabarani kuwa ni moja ya chanzo cha kutokea kwa ajali hizo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Mnyakongo shuleni Bw. Moses Patson amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo kwa muda mrefu licha ya kufikisha malalamiko hayo kwa viongozi wa ngazi za juu lakini bado utekelezaji wake umekuwa mdogo na athari nyingi zikiendelea kutokea.

Dodoma FM Habbari imezungumza na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa Mhandisi Ngusa Izengo juu ya changamoto hiyo na kukiri kuwepo kwa ubovu wa makutano ya barabara hizo huku akieleza kuwa barabara hiyo iko chini ya wakala wa barabara nchini (TANROADS) na wao kama Halmashauri wamekwisha wasiliana na Tanroads kwa ajili ya utekelezaji wa zoezi hilo.

Na Pius Jayunga                                                       Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...