Skip to main content

TANZANIA YAADHIMISHA MAADHIMISHO YA HALI YA HEWA NA KUITAKA JAMII KUWA NA IMANI NA UTABIRI UNAOTOLEWA


                                  Image result for maadhimisho ya hali ya hewa




Imeelezwa kuwa ili kuondokana na majanga mbalimbali ikiwemo mafuriko na ukame mamlaka husika na jamii zinapaswa kutunza mazingira ipasavyo ikiwa ni pamoja na miundombinu iliyopo nchini.


Waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano profesa Makame Mbarawa ameyasema hayo leo mjini Dodoma katika kusherehekea siku ya mamlaka ya hali ya hewa duniani ambapo amesema jamii inapaswa kutunza mazingira ili kupunguza changamoto za mafuriko na ukame.

Amesema jamii na mamlaka husika zinatakiwa kuchukua tahadhari pindi zinapopata taarifa za mamlaka ya hali ya hewa kwa kuandaa miundombinu rafiki itakayoweza kuzuia maafa kutokea.

Katika kufanikisha hayo Waziri  Mbarawa amesema serikali itaendelea kuiwezesha mamlaka ya hali ya hewa kwa kila hali ili iendelee kutoa taarifa za uhakika zitakazosaidia kukuza uchumi katika nchi.

Nae mkurugenzi wa mamlaka ya hali ya hewa nchini Agnes Kijazi amesema mamlaka ina vifaa vinavyowezesha kutoa taarifa za usahihi na kwamba kwa mujibu wa makubaliano ya kimataifa utabiri ukiwa na usahihi wa 70% unaweza kutumika kwa maendeleo.

Mamlaka ya hali ya hewa imeazimisha miaka 68 tangu kuanzishwa duniani ambapo ilianzishwa march 23 mwaka 1950 na  kwa Tanzania mamlaka hii ilianzishwa mwaka 1999 ,na imebebwa na kaulimbiu JIWEKE TAYARI NA ZINGATIA TAARIFA ZA HALI YA HEWA.

Mariam Matundu                                                            Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...