Skip to main content

TANZANIA NI NCHI YA 6 KWA IDADI KUBWA YA WATU BARANI AFRIKA





                                           Image result for POPULATION





Siku moja baada ya waziri wa fedha na mipango Dr. Philip Mpango kutoa takwimu za makisio ya idadi ya watu Nchini Serikali imeshauriwa kuwekeza katika sekta ya kilimo na viwanda ili kuendana na idadi ya ongezeko la watu.

Mchambuzi wa masuala ya uchumi kutoka chuo kikuu cha Iringa Pr. Enock Wiketye ameiambia Dodoma fm kuwa ongezeko la watu Nchini linapaswa kwenda sambamba na kukua kwa uchumi Nchini ili kukidhi mahitaji.

Amesema uzalishaji mali unapaswa kuimarishwa katika sekta ya kilimo na viwanda kwa kuwawezesha wakulima kuendesha kilimo chenye tija tofauti na ilivyo kwa sasa ambapo 70% ya wakulima wanaendesha kilimo cha jembe la mikono, 20% wakiendesha kilimo cha jembe la kukokota na ng’ombe huku 10% pekee wakiendesha kilimo cha kukokota na trekta.

Kwa mjibu wa taarifa ya makisio ya idadi ya watu iliyotolewa na waziri wa fedha na mipango Dr. Phillip Mpango inaonesha viwango vya uzazi na vifo kwa takwimu za mwaka 2016, idadi ya watu nchini ikiwa ni milioni 54.2 ambapo Tanzania Bara ni watu milioni 52.6  na Tanzania visiwani watu milioni 1.6 kwa mwaka 2018.

Kutokana na makisio hayo Prof. Wiketye amesema idadi ya watu waliopo Nchini sehemu kubwa ikiwa ni kundi la vijana ambao wanahitaji kupata ajira ili kujipatia kipato kupitia sekta mbalimbali hivyo ni muhimu kwa Serikali kuweka mikakati thabiti ya kukuza uchumi kupitia sekta ya kilimo na viwanda.

Tanzania inakuwa nchi ya 6 kwa idadi kubwa ya watu Barani Afrika baada ya Nigeria, Ethiopia, DRC pamoja na Misri kuwa na idadi kubwa ya watu.
Na Pius Jayunga                                                      Dodoma Fm

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...