Skip to main content

TAIFA STARS KUWAVAA ALGERIA SAA MBILI USIKU


                       
Kikosi cha Taifa Stars kinashuka Uwanjani 'Mustapha Tchaker Stadium' kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Algeria jioni ya leo huko Blida, nchini humo.

Mchezo huo ambao ni wa kalenda ya FIFA, utakuwa unaipa nafasi Tanzania ya kulipiza kisasi baada ya kupoteza kwa mabao 7-0 wakati timu hizo zilipokutana mara ya mwisho 2015.

Tanzania ilifungwa idadi hiyo ya mabao wakati wa kuwania kufuzu kuelekea michuano ya Kombe la Dunia kuelekea Urusi mwaka huu.

Licha ya kufungwa, timu zote hazijafanikiwa kufuzu kushiriki michuano hiyo inayotarajia kuanza miezi kadhaa ijayo.
Lakini wakati hayo yakijiri ni kwamba shirikisho la soka tz limeanza mchakato wa kutafuta kocha mpya wa kukinoa kikosi cha starz kutokana mkataba wa salum mayanga kufika ukingoni
Kikosi cha Taifa Stars kitakachoanza dhidi ya Algeria, mchezo wa kirafiki

1. Aishi Manula
2. Shomary Kapombe
3. Gadiel Michael
4. Abdi Banda
5. Kelvin Yondani
6. Himid Mao
7. Saimon Msuva
8. Mudathir Yahya
9. Mbwana Samata
10. Said Ndemla
11. Shiza Kichuya


Kikosi cha akiba

12. Ramadhan Kabwili
13. Abdulrahman Mohamed
14. Hassan Kessy
15. Erasto Nyoni
16. Abdulazizi Makame
17. Mohamed Issa
18. Feisal Salum
19. Ibrahim Ajib
20. Shaaban Iddi
21. Yahya Zayd
22. Rashid Mandawa

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...