Skip to main content

TAHADHARI YATOLEWA DHIDI YA UGONJWA WA NGIRI MAJI


                                           Image result for UGONJWA WA NGIRI MAJI



Wananchi wakumbushwa kusafisha mazingira na kutumia vyandarua vyenye dawa ili kuepuka ugonjwa wa ngiri maji unaosababishwa na mdudu aina ya mbu.

Hayo yameelezwa na daktari  kutoka  kituo cha afya cha Makole manispaa ya Dodoma  DR.GRAYSON JULIUS NDALAMA  wakati akizungumza  na Dodoma FM  ambapo amesema ugonjwa wa Ngiri maji ni kama malaria na kuwasihi wananchi wazingatie usafi katika mazingira yanayo wazunguka  na kutumia vyandarua kwa umakini.

Hata hivyo Dokta GRAYSON amesema awali ugonjwa huo ulikuwa unawapata kwa kiasi kikubwa watu wa pwani lakini sasa hivi imekuwa tofauti kwani  ugonjwa huo unaweza kumpata mtu kutoka sehemu yoyte.

Dokta GRAYSON amesema ugonjwa huo ni miongoni mwa magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele na kuongeza kuwa ugonjwa huo unawakuta watu wenye maisha ya hali ya chini huku akisema hauchagui jinsia.

Pamoja na hayo amesema wana kampeni ya kugawa dawa kwa ajili ya kinga tiba ya ugonjwa huo ambayo unatakiwa kumeza kila baada ya miezi mitatu.

Kulingana na takwimu za mwaka 2016  serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ilisema watu milioni 47 wapo katika hatari ya kupata magonjwa ya Matende, Ngiri Maji na Kichocho nchini Tanzania huku wengine milioni 6 wakiwa katika hatari ya kupatwa na ugonjwa wa usubi.

Na Benard Filbert                                                            Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...