Skip to main content

SUMATRA INATARAJIA KUFANYA MABADILIKO MAKUBWA MKOANI DODOMA.


                                    Image result for Daladala dodoma


Mamlaka ya udhibiti usafirishaji wa nchi kavu na majini SUMATRA inatarajia kuanza kutoa leseni kwa makampuni na vyama vya ushirika mkoani Dodoma ili kuboresha huduma za usafiri hasa wa daladala.

Maazimio hayo yamekuja kufuatia kikao cha wamiliki wa daladala na SUMATRA mkoani Dodoma ambapo imeleezwa kuwa kwa kufanya hivyo itasaidia kuboresha usafiri huo ili kuendana na mabadiliko ya kuijenga makao makuu.

Akizungumza katika kikao hicho meneja leseni SUMATRA  Leo John Ngowi amesema kuwa mpaka kufikia April Mosi mamlaka inatarajia kuanza kutoa leseni katika makampuni ili kutoa huduma ya usafiri sambamba na kufuta vituo vya daladala vilivyopo mjini na badala yake daladala zifanye mzunguko.

Aidha amesema kuwa kutokana na mji wa Dodoma kuwa na ongezeko la watu SUMATRA imeamua kuwa na magari aina ya costa zitakazofanya kazi ya kusafirisha abiria katikati ya mji na daladala zitapelekwa pembezoni mwa mji.

Baadhi ya wamiliki wa daladala wamepata wasiwasi juu ya umbali kutoka kituo kimoja hadi kingine lakini pia biashara ya mzunguko bila kukaa katika kituo kimoja huenda ikaharibu biashara yao kwa kupata hasara.

Akijibu hoja hizo afisa mfawidhi sumatra amesema kuwa kwasasa hakuna haja ya kujadili juu ya hilo bali ni kuanza kuutumia mfumo huo na iwapo kasoro zitajitokeza watajua namna ya kukabiliana nazo.

Mariam Matundu                                                                 Dodoma FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...