Skip to main content

SIMBA SC: TUKO TAYARI KUWZIMA AL AMSRY KESHO TAIFA

                          

NAHODHA wa Simba SC, John Raphael Bocco amesema kwamba wapo tayari kucheza vizuri na kwa bidii kesho dhidi ya Al Masry ili washinde.

  Simba SC wanawakaribisha Al Masry kesho kuanzia Saa 12:00 jioni Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza ya Kombe la Shirikisho la Soka Afrika.

  Na kuelekea mchezo huo, Kocha Mkuu, Mfaransa, Pierre Lechantre na Nahodha wa timu, Bocco walijitokeza kuzungumza na Waandishi wa Habari asubuhi ya leo ukumbi wa mikutano ofisi za Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

 

Katika mkutano huo, kocha Lechantre alisema baada ya maandalizi mazuri, vijana wake wapo tayari kwa mchezo wa kesho.

 
Nahodha, Bocco kwa upande wake alisema anafahamu utakuwa mchezo mgumu kwa sababu Al Masry ni timu nzuri kwa rekodi zake na matokeo yake ya nyuma.
Lakini Bocco akasema hata Simba ni timu nzuri na iona rekodi nzuri pia kwenye michuano ya Afrika, hivyo mchezo wa kesho utakuwa wa ushindani mkubwa.

 
Bocco amewaomba wapenzi wa Simba kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Taifa kesho kuishangilia timu yao ili iweze kupata ushindi nyumbani.   

 
Baada ya mchezo wa kesho, timu hizo zitarudiana siku 10 baadaye mjini Cairo, Misri na mshindi wa jumla ataingia kwenye mchujo wa kuwania kuingia hatua ya makundi kwa kucheza na moja ya timu zilizotolewa kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika.

 
Timu zinazoingia hatua ya makundi Kombe la Shirikisho hupatiwa dola za Kimarekani 150,000 zaidi ya Sh. Milioni 300 ambazo huongezeka kulingana na matokeo zaidi kuanzia hatua hiyo.

 
Bingwa wa Kombe la Shirikisho hupata Dola za Kimarekani 625,000 zaidi ya Sh. Bilioni 1.5, mshindi wa Pili wakati mshindi wa pili wa Kundi hupata dola 239,000 sawa na wa tatu wakati mshindi wa nne hupata dola 150,000.

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...