Skip to main content

SERIKALI YAKIRI KUWEPO KWA UGONJWA WA DENGUE NCHINI

                   Image result for HOMA YA DENGUE


Serikali imekiri kuwepo kwa ugonjwa wa Dengue baada ya kukamilika kwa vipimo vilivyofanywa katika maabara ya Taifa kufuatia kupokelewa sampuli kumi na tatu za damu kutoka Hospital ya International School of Tanganyika (IST) iliyopo Jijini Dar es salaam.

Waziri wa Afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh. Ummy Mwalimu ameyasema hayo March 21,2018 wakati akizugumza na waandishi wa habari na kueleza kuwa kati ya sampuli kumi na tatu za damu zilizofanyiwa vipimo sampuli kumi na moja zilionesha kuwa na ugonjwa wa Dengue.

Kufuatia kuwepo kwa ugonjwa huo Nchini Serikali kupitia wizara ya Afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto imetoa taarifa kwa waganga wakuu wa Mikoa na Wilaya Tanzania Bara ili kuzitambua dalili za ugonjwa huo na kwamba ugonjwa wa dengue uliwahi kuripotiwa hapa Nchini mwaka 2010, 2013 na 2014.

Waziri Ummy amesema homa ya Dengue inasababishwa na virusi vinavyoenezwa na mbu aina ya Aedes weusi walio na madoa meupe yanayo ng’aa huku dalili za ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na homa ya ghafla, kuumwa kichwa hususani sehemu za macho, maumivu ya viungo na uchovu, na dalili hizo huanza kujitokeza kati ya siku 3 hadi siku kumi na nne tangu mtu alipoambukizwa.

Aidha Waziri Ummy amesema kutokana na kuwepo kwa ugonjwa huo hakuna vikwazo vyovyote vilivyotolewa kwa wasafiri wanaoingia na kutoka Nchini na kwamba shughuli za usafiri wa kuingia na kutoka Nchini zinaendelea huku jitihada mbalimbali zikichukuliwa ili kutokomeza ugonjwa huo.

Na Pius Jayunga                                                             DODOMA FM

Comments

Popular posts from this blog

WAJAWAZITO WASHAURIWA KUTUMIA VIDONGE VYA FOLIC ACID KUEPUKA WATOTO VILEMA

                                                                  Mama wajawazito wameshuriwa kutumia dawa aina ya FOLIC ACID katika kipindi cha miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito ili kuepuka kupata mtoto mwenye   mapungufu. Rai hiyo imetolewa na Daktari kutoka Hospitali ya Matovyolwa mjini Dodoma   Dk.MUBARACK ISSA ALI wakati akizungumza na Dodoma FM juu ya athari zitokanazo na mama kutotumia dawa hizo. Dr Mubarack amesema katika kipindi cha ujauzito mama huwa anapitia changamoto nyingi hivyo ni vyema akatumia dawa aina ya FOLIC ACID ili kuepuka kupata mtoto mwenye tatizo la mgongo wazi, kichwa kikubwa pamoja na upungufu wa damu. Aidha Dk. Mubarack amesema   ili kuepuka kupata mtoto njiti   kipofu na kusababisha kifo kwa mtoto   ni vyema mama akaepuka matumizi ya pombe, dawa za kulev...

MIKOA INAYOONGOZA KWA UKEKETAJI TANZANIA YATAJWA

Mila potofu   katika jamii ya kimasai imetajwa kuwa changamoto kwa maafisa ustawi wa jamii wa halimashauri ya wilaya ya Ngorongoro  kutokana na kukosa ushirikiano wa kutatua Tatizo la ukeketaji kwa jamii hiyo. Akizungumza na waandishi ya habari Afisa Ustawi Wa jamii Bwana ALOYCE  LOLIKISWALI katika semina iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu Sanyansi na Utamaduni UNESCO kwa lengo la kupinga ukeketaji wa wanawake amesema kukosekana kwa ushirikiano kwa jamii imekuwa ni changamoto ambayo imepelekea kushindwa kudhibiti ukeketaji pamoja na ukatili wa kijinsia. Kwa upande wake Mwenyekiti wa Malaigwanan Bwana JOSEPH TIRIPAI amebainisha kuwa mila na desturi zao zitabadilika kulingana na wakati lakini watahakikisha wanalinda watoto wanaozaliwa kutokeketwa na kusisitiza elimu kuendelea kutolewa hususani shuleni. Katika hatua nyingine mratibu wa afya ya mama na mtoto ameeleza kuwa wanawake wajawazito waliokeketwa wanalazimika   kujifug...

MITI YA KIVULI MAARUFU KAMA PANGA UZAZI YAZUA TAHARUKI WILAYANI BAHI DODOMA

                                                  Mganga Mkuu wa Wilaya ya Bahi Jijini Dodoma Dk.Philipina Philipo amewatoa hofu wakazi   wa Wilaya hiyo juu ya taarifa za kuwepo kwa madhara katika miti ya kivuli maarufu kama PANGA UZAZI ambayo imezua hofu kwa wananchi hao. Hoja hiyo imeibuliwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa halmashauri hiyo ambapo baadhi ya madiwani wameomba kupatiwa ufafanuzi kuhusu kuwepo kwa fununu kuwa mti huo una madhara na kuongeza kuwa baadhi ya wananchi wameanza kuikata wakihofia kupatwa na madhara hayo. Akitoa ufafanuzi kuhusu miti hiyo Mganga Mkuu wa Wilaya Dk.Philipina Philipo amesema hadi hivi sasa hakuna utafiti wowote uliofanyika na kubainisha kuwa mti huo hauna madhara hivyo wananchi hawana haja ya kuhofia chochote. Kutokana na Majibu hayo ya DK PHILIPINA yamepelekea kuibua kwa hoja nyingine kwa madi...